• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri Jafo awahurumia watoto wa kijiji cha Olkejunderet kata ya Olkokola

Posted on: March 18th, 2018

Waziri wa Nchi-OR TAMISEMI mhe. Selemani Jafo amewahurumia cha watoto wa kijiji cha Olkejundereti kata ya Olkokola na kusikitishwa na kitendo cha watoto hao kutembea umbali wa zaidi ya Kilomita kumi kwenda shuleni kutokana na kijiji chao kukosa shule ya msingi.

Masikitiko hayo yamekuja baada ya kutembelea ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu, vilivyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi kwa lengo la kuanzisha shule mpya ya Msingi Olkujunderet kuwezesha watoto kupata elimu karibu na maeneo wanayoishi.

Akizungumza mbele ya waziri Jafo, Diwani wa kata ya Olkokola, mheshimiwa Kalanga Laiza, amesema kuwa wamelazika kuanza ujenzi wa shule ya msingi katika eneo hilo, baada ya kuona watoto wanateseka kutembea umbali mrefu kufuata elimu.

Diwani Kalanga amefafanua kuwa, kijiji hicho ni kipya na baada ya kugawanya kikajikuta hakina shule wala ofisi ya kijiji, hivyo wananchi kuamua kununua eneo la kujenga ofisi na shule.

Ameongeza kuwa wananchi wamechanga fedha na kununua eneo la Ekari 10, na kuanza kujenga vyumba viwili vya madarasa ili waanze kwanza kusoma watoto wenye umri mdogo, huku wakiendelea kutafuta nguvu za kumalizia mdarasa mengine na kufikia madarasa nane kama sheria ya kuanzisha shule inayotaka.

" Watoto wanapata shida sana, hasa wakati huu wa mvua ambapo makorongo yanajaa maji, na kusababisha kushindwa kuhudhuria masomo kwa kuepusha madhara yanayoweza kuwapata kutokana na mvua" amesema Kalanga

Hata hivyo Waziri Jafo, amemuagiza mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, kutafuta fedha haraka kumalizia ujenzi huo na kuahidi serikali pia itaweka mikakati ya kuhakikisha miundo mbinu ya shule hiyo inakamilika na ifikapo Januari 2019, watoto waanze kusoma shuleni hapo.

Ameongeza kuwa kutokana na umbali huo na hali ya hewa ya maeneo hayo, ni dhahiri kuna uwezekano wa watoto kutokuandikishwa shule, na kuzorotesha haki ya mtoto kupata elimu na sera ya elimu ya kila mtoto mwenye umri wa kuanza shule aandikishwe.

"Inakatisha tamaa ya kupenda shule kwa mtoto wa miaka sita na saba anayeanza shule kutembea Kilomita kumi na zaidi, mkurugenzi, zinatakiwa hatua za haraka za ukamilishaji wa ujenzi shule hii, ili watoto wetu wasiendelee kuteseka kutembea umbali huo" amesisitiza Waziri .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.