• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri Jafo awaongeza wakazi wa Halmashauri ya Arusha kwa kujitoa kuchangia ujenzi wa miaradi ya maendeleo katika maeneo yao

Posted on: March 16th, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za mheshiwa Selemani Jafo amewapongeza wananchi wa halmashauri ya Arusha kwa kuchangia kwa hali na mali miradi ya maendeleo katika maeneo yao, na kuwataka wananchi wengine kuiga mfano huo.

Waziri Jafo ametoa pongeza hizo baada ya kuridhishwa na kuguswa na ujenzi wa kituo cha afya cha Ilkurot kata ya Olkokola kilichojengwa kwa nguvu za wananchi kwa kuchangishana wao kwa wao.

Waziri Jafo amethibitisha kuridhishwa sana na wananchi wa halmashauri ya Arusha kuchangia ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo kisekta, na kudhihirisha kuwa michango hiyo huiongezea nguvu serikali yao kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

"Ninaridhishwa sana na juhudi za wananchi wa halmashauri hii katika kuchangia miradi ya maendeleo, serikali inatambua na kuthamini juhudi zenu wananchi, kufuatia juhudi hizo, serikali imetoa shilingi milioni 500 za kumalizia ujenzi wa kituo cha Afya Nduruma na zimesimamiwa vizuri, kituo hicho kilianza kujengwa na wananchi wa Nduruma, hata kituo hiki cha Ilkurot serikali itaongeza nguvu hapa" amesema Waziri Jafo.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa kituo cha Afya Ilkurot mbele ya Waziri Jafo, Afisa Mtendaji wa kijiji Ilkurot, Charles Sikoi, amesema kuwa wananchi wa kijiji hicho wamechanga kiasi cha shilingi milioni 30 na kuanza ujenzi huo kutokana na adha ya upatikanaji wa huduma ya afya katika eneo hilo.

Ameongeza kuwa mpaka kukamilika kwa jengo hilo, zinahitajika jumla ya shilingi milioni 96.6 na mpaka sasa jengo hilo limetumia shilingi milioni 29 ikiwa ni pamoja na vifaa vya ujenzi mpaka jengo hilo kufikia hatua ya boma.

Hata hivyo waziri Jafo amesema kuwa serikali itafanya jitihada za kuhakikisha ukamimilishaji wa jengo hilo unafanyika na kusisitiza kuwa mpaka kufikia mwezi Disemba,2018 jengo hili liwe limekamilika na wananchi waanze kupata huduma.

Ameongeza kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya chenye hadhi ya nyota tano, chenye kulaza wagonjwa, jengo la kujifungulia, maabara, jengo la upasuaji na jengo la maiti 'mortuary' na vituo hivyo kuwa na dawa za kutosha.

Naye kaimu mkurugenzi halmashauri ya Arusha Paulus Kessy amesema kuwa, katika bajeti ya mwaka 2018/19, halmashauri imepanga bajeti ya shilingi milioni 10 kwa mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya uendelezaji wa miundombinu ya kituo hicho cha afya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.