• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri Lugola akumbusha Jeshi la Polisi Arusha DC matumizi sahihi ya sheria

Posted on: February 16th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Serikali kupitia wizara ya mambo ya Ndani ya nchi, imewahakikishia wananchi katika halmashauri ya Arusha,  ulinzi na usalama  kwa asilimia miamoja, kwa kuwa hilo ni jukumu la serikali yao.

Wananchi hao, wathibishiwa Usalama huo na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Nchi, Mhe. Kange Lugola, wakati akiwahutubia wananchi wa halmashauri hiyo, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya kituo cha mabasi Ngaramtoni na kuahidi kuanzisha wilaya ya kipolisi Ngaramtoni kutokana na ukuaji wa mji na ongezeko la idadi ya watu.

Akiwahutubia wananchi hao,  pamoja kupokea kero na changamoto za wananchi, Waziri Lugola amesema kuwa, jukumu kubwa la serikali ni kuwapa haki na kuwahakikishia usalama wananchi wao bila kuwaonea wala kubagua.

Aidha amesema kuwa, serikali inatambua kuwa kuna baadhi ya watumishi wa jeshinla polisi ambao si waaminifu, bado hawatendi haki stahiki kwa wananchi, na kufanya hivyo ndio wanalichafua jeshi hilo na kuongeza kuwa serikali inaendelea na opereshi ya kuwaondoa.

Amewataka askari kufanya kazi zao kwa uaminifu kwa kufuata misingi na maafili ya kazi, ikiweomo kuacha kuwabughudhi wananchi hasa wakiwa katika maeneo yao ya kazi huku wakiendelea na shughuli zao halali.

Kangi Amepiga marufuku ukamataji wa waendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda na kufungia pikipiki zao polisi bila sababu za msingi hasa kwa makosa madogo madogo ambayo yanasababisha kero na bughudha kwa wananchi na familia zao.

Ameyataja makundi ya makosa yanayopaswa kukamatwa na polisi ni  bodaboda zilizojihusisha na uhalifu wa aina yoyote, bodaboda zilizosababisha ajali pamoja na bidaboda isiyokuwa na mwenyewe.

Hata hivyo amewataka wananchi kushirikiana na jeshi la polisi kulinda amani na usalama wao kwa kutii sheria bila shurti, kuacha tabia ya kuvunja sheria pamoja na kuacha tabia ya kutoa rushwa wajati wa kupata dhamana kwa watu waliokamatwa kwakuwa dhamana ni haki ya mtuhumiwa.

Katika mkutano huo, Waziribhuyo wa mambo ya Ndani nchini, ametoa gari kwa kituo cha Polisi Ngaramtoni na kumkabidhi mkuu wa kituo cha Polisi Ngaramtoni Bariki Kileo, na kuongeza kuwa gari hilo litumike kuwahudumia wananchi na kuhakikisha usalsma wa wananchi upatikana kwa asilimia mia moja.

Awali akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Arumeru, mbunge wa vuti Maalum Taifa, Mhe. Amina Mollel ameeleza kuwa kumekuwepo na askari wasiokuwa waaminifu wanaowanyanyanyasa vijana waendesha bodaboda kwa kuwakamata wao kinyume na sheriq pamoja na kufungia pikipiki zao, ilihali vijana hao wanazitegemea pikipiki hizo kwa ajili ya uzalishaji na kuendeshea maisha yao.

Katika Mkutano huo Mkuu wa Wilaya Ya Arumeru Mheshimiwa Jeri Cornel Muri alimuhakikishia Waziri huyo na wananchi wa Wilaya kwa ujumla kuwa wilaya hiyo imejipanga kukabiliana na changamoto zote za wananchi pamoja kuthibiti viashiria vyote vya Uhalifu

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya pia ameeleza kuwa tayari wilaya hiyo imefanikiwa kuwapata wadau wa Maendeleo watakaosaidia kuyakarabati magari yote mabovu ya Jeshi la Polisi katika wilaya hiyo ili iweza kulisaidia Jeshi la polisi kuimarisha Doria wilayani humo

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.