• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: TATUENI MIGOGORO KWA NJIA MBADALA. KUONDOA UADUI NA KUPUNGUZA UMASIKINI

Posted on: September 9th, 2022

Na Elinipa Lupembe 

Jamii imetakiwa kujifunza kutatua migogoro baina yao kwa njia mbadala, njia ambayo licha ya kuwa haina gharama kubwa, huleta amani kwa kupunguza uadui na kuondoa umasikini miongoni mwa wahusika ndani ya jamii.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, wakati akifungua Kampeni ya  utoaji msaada wa Kisheria bure kwa wananchi, inayofanyika katika kata ya Ilkiding'a, halmasahuri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.

Dkt. Ndumbaro amefafanua kuwa, Wizara yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, inao utaratibu wa kutoa msaada wa kisheria bure kwa wananchi, kwa  kufanya usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala, lengo likiwa ni kuleta amani baina ya wahusika pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji wa kesi.

"Tunafahamu kuendesha kesi mahakamani kunahitaji gharama kubwa za kuweka mawakili, gharama ambazo wananchi wengi hushindwa kuzimudu na kukosa haki zao huku wakibaki na majeraha mioyoni mwao, kupitia kampeni hii, tunatoa msaada wa kisheria bure na kuhakikisha tunafanya usuluhishi kwa njia ya amani" Amefafanua Dkt Ndumbaro.

Aidha amebainisha kuwa utoaji wa huduma za kisheria bure, wizara yake inatekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020, ibara ya 120 kifungu D inayoelekeza kuimarisha mfumo wa usajili ili kutoa msaada wa kisheria bure, hususani kwa wananchi waiso na uwezo wa kumudu gharama za kuweka mawakili kusimamia kesi zao.

Naye Katibu Tawala mkoa wa Arusha, Missaile Musa, licha ya kuishukuru serikali kupitia wizara hiyo, amemuomba mheshimiwa Waziri, kampeni hiyo kufanyika katika wilaya zote za mkoa wa Arusha, kutokana na ukweli kwamba, mkoa huo unakabiliwa na migogoro mingi hususani ya ardhi na mipaka.

"Nikuombe mheshimiwa Waziri, kampeni hii isiishie hapa, ifanyike kwenye wilaya zote za mkoa wa Arusha, tuna uhitaji mkubwa wa msaada wa kisheria kwa wananchi wetu, wananchi wana migogoro ya ardhi na mipaka katika maeneo mengi, kupitia jukwaa hili, ninaamini migogoro mingi itatatuliwa na kurejesha amani miongoni na wananchi wetu".Amesisitiza Katibu Tawala huyo.

Hata hivyo Waziri Dkt. Ndumbaro, licha ya kukubali ombi hilo la Katibu Tawala, amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara yake, kuratibu jambo hilo katika mkoa wa Arusha na kwenda mbali zaidi kwa kufanya kampeni hiyo katika halmashauti zote nchini.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mheshimiwa Ojung'u Salekwa, amemuomba pia mheshimiwa Waziri, kupata wasaidizi wa Kisheria katika halmashauri hiyo, kwa kuwa ni huduma inayohitajika sana, kutokana na uwepo wa migogoro mingi na baadhi ya wananchi kupoteza haki zao kwa kushindwa kumudu gharama za uendeshaji wa kesi.

"Mheshimwa Waziri, wananchi wa halmashauri hii, wanakabiliwa na migogoro mingi ya kisheria ikiwemo migogoro ya ardhi na mipaka, kesi za ukatili na ubakaji, urithi na mirathi, ukandamizwaji wa wanawake na watoto, madhila ambayo kiuhalisia yanaondoa amani na utulivu miongoni mwa jamii, uwepo wa msaada wa kisheria bure, utatusaidia kutatua migogoro mingi" Amebainisha Mheshimiwa Mwenyekiti.

Awali, wananchi waliofika katika kampeni hiyo, wameipongeza Serikali na Wizara ya Sheria kwa kuona umuhimu wa kufanya kampeni hiyo, jambo ambalo licha ya kupata msaada lakini limewawezesha wananchi kujifunza mambo mengi juu ya upatikanaji wa haki zao kwa njia ya amani bila kuwa na migogoro wala uhasama miongoni mwao.

Jacob Lembris mkazi wa Sambasha, amesema kuwa kampeni hiyo imewafungua ufahamu wa namna bora ya utatuzi wa migogoro, usuluhishi nje ya mahakama, njia sahihi za kupata haki iliyopotea pamoja na kutambua umuhimu wa haki za watoto na wajibu wa wazazi kwa watoto wao.

Kampeni ya Kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi bure,  yenye kauli mbiu ya "Utatuzi wa Migogoro kwa njia Mbadala, hupunguza Uadui na kuziua umaskini", inafanyika kwa siku mbili katika kata ya Ilkiding'a, ikijumuisha wakazi wa kata hiyo na kata za jirani za Sambasha, Olturoto na Kiranyi.


ARUSHA DC 

TUPO KAZINI ✍✍✍



Waziri wa Sheria na Katiba, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, akizungumza na wanachi wa halmashauri ya Arusha wakati akifungua Kampeni ya Utoaji Msaada wa Kisheria bure, katika viwanja vya kanisa la KKKT kata ya Ilkiding'a.



Katibu Tawala mkoa wa Arusha, Massaile Musa, akizungumza mble ya mgeni rasmi na Waziri wa Sheria na Katiba , wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Utoaji Msaada wa Kisheria bure, katika viwanja vya kanisa la KKKT kata ya Ilkiding'a,.


Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u Sallekwa, akizungumza mble ya mgeni rasmi na Waziri wa Sheria na Katiba , wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Utoaji Msaada wa Kisheria bure, katika viwanja vya kanisa la KKKT kata ya Ilkiding'a.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.