# Apongeza juhudi za wananchi wa halmashauri ya Arusha kwa kujitoa kuchangia kwa hali na mali ujenzi wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, na kuwataka watanzania wengine kuiga mfano huo.
# Uchangiaji huo umeanza kuondoa kasumba ya watanzania kusubiri wageni kutoka Ulaya kutujengea miradi ya maendeleo yetu binafsi. Zaidi ameridhishwa na hatua ya wananchi wa kijiji cha Ilkurot kuanza ujenzi wa kituo cha afya ndani ya kijiji chao kwa kuchangishana wenyewe, kituo ambacho kitahudumia wakazi wa kata nzima ya Olkokola.
# Serikali itaandaa mipango ya kuongezea nguvu na kuhakikisha kituo kinakamilika na kuanza kufanya kazi mwishoni mwa mwaka huu 2018, ili kuunga mkono juhudi za wananchi wa Ilkurot.
# Wananchi wa Ilkurot wana sababu ya msingi kujenga kituo cha afya,kutokana na changamoto ya kutembea Kilomita 16 mpaka 20 kupata matibabu kwenye hospatali ya Seliani Ngaramtoni, hospitali ya wilaya Olturumet na hospitali ya mkoa Mount Meru.
# Lengo la serikali ya awamu ya tano,ni kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya, na mwananchi apate huduma ya afya ndani ya kata yake.
# Serikali imeanza kwa kuboresha miundo mbinu ya vituo vya afya 250 na kuwa na hadhi ya nyota tano, kwa kukujenga maabara, wodi za kulaza wagonjwa, wodi za wazazi,jengo la upasuaji na jengo la kuhifadhia maiti.
# Serikali ilitoa shilingi milioni 500 kuboresha miundo mbinu ya kituo cha afya Nduruma ndani ya halmashauri hii baada ya kuridhishwa na juhudi za wananchi hao kujenga kituo hicho kwa nguvu zao, hata baada ya kupeleka fedha, wananchi walijitoa kwa hali na mali kusimamia ujenzi huo, kituo sasa kiko hatua za mwisho kukamilika.
# Serikali ya awamu ya tano imeongeza bajeti ya dawa na kurahisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali zake za serikali kwa kuboresha bohari ya dawa ya taifa 'MSD'.
#Amuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha kutafuta pesa kuongeza nguvu za ujenzi wa kituo hicho cha Afya.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.