• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Arusha DC yaadhimisha Siku ya hedhi huku jamii ikitakiwa kuvunja ukimya na kuondoa vikwazo

Posted on: May 28th, 2018

Halmashauri ya Arusha imeadhimisha siku ya hedhi duniani huku jamii ikitakiwa kuvunja ukimya kwa kupaza sauti itakayoondoa usiri utakaomuwezesha mwanamke kuwa na mazingira bora yatakayomuwezesha kuwa hedhi salama.  

Maadhimisho hayo yaliyofanyika kwenye shule ya sekondari Mukulat, kata ya Lemanya na kushirikisha zaidi ya wanafunzi 500 kutoka shule tano za sekondari na shule mbili za msingi zilizo karibu na shule ya sekondari Mukulati.

Akizingumza wakati wa maadhisho hayo, Afisa Afya halmashauri ya Arusha, Issa Msumari amesema kuwa jamii inalazimika kuondokana na mila na desturi za usiri kuhusu hedhi na kuanza kuwa wazi ili kuweka mazingira salama ya kipindi chote atakapokuwa kwenye siku za hedhi.

Ameongeza kuwa wanawake wengi wamejikuta wakipata madhara ya kiafya, kisaikolojia na hata kiuchumi kutokana  na hedhi isiyo salama inayotokana na usiri uliyopo ndani ya jamii.

Afisa Afya huyo ameyataja madhara yanayoweza kutokana na hedhi isiyo salama ni pamoja na maumivu makali, muwasho, michubuko, fungusi, maambukizi kwenye via vya uzazi pamoja na maambukizi kwenye njia ya mkojo UTI.

Hata hivyo amewataka wazazi na walezi, kuzungumza na watoto wa kike juu ya umuhimu wa hedhi salama bila kuona aibu sambamba na kuwawezesha kupata vifaa salama vya kujihifadhi wakati wakuwa kwenye hedhi.    

Ni jukumu la jamii kuwawezesha wanawake hasa wasichana, kupata vifaa vya kutumia wakati wote wa hedhi, kuwa na utaratibu wa maeneo maalumu ya kujisitiri wakati wa kubadilisha vifaa namahali salama pa kutupa vifaa vilivyotunika,  hii itamuwezesha mwanamke kuwa mkamilifu kipindi chote cha hedhi.  

"Jamii inapaswa kutambua hedhi inahitaji rasilimali nyingi ikiwemo fedha ya kununua vifaa salama vya kujisitiri, inahitaji miundombinu mizuri ya kujihifadhi na kuanika vifaa visivyotumika mara moja, na inahitaji eneo la kuviteketeza baada ya kutumika, wanawake peke yao hawataweza" amesema Msumari  

Aidha wanafunzi walioshiriki kwenye maadhimisho hayo, wamefurahia maadhimisho ya siku hiyo ya hedhi na kusema kuwa mafunzo waliyoyapata yamewawezesha kupata ujasiri na kujiamini siku zote za hedhi, tofauti na hapo awali walikuwa wanaona aibu, kuzungumzia suala zima la hedhi hata wakati mwingine mbele ya wasichana wenzao.

Mwanafunzi Judith Sikulumbwe amesema kuwa kupitia siku hiyo rasmi kwa wasichana na wanawake, amepata mwanga zaidi wa kuvunja ukimya na kuwa wazi pamoja na kutambua namna ya kujihifadhi, muda wa kuvaa vifaa hivyo, namn kuteketeza vifaa vilivyotumika,  na kujihakikishia usafi binafsi.

Hata hivyo mwanafunzi, Pendo Frank amesema kuwa amefurahia elimu waliyoipata na itawasaidia kuanzisha klabu kwenye shule zao, ambazo zitawafanya kuwa huru kujadili masuala ya hedhi salama na kuwafundisha wenzao kwa kushirikushana na walimu na walezi wa shule 'matron'.

Naye mratibu wa miradi, shirika la WaterAid Tanzaniam Upendo Muntambo amesema kuwa,  ingawa mila na desturi zinafanya hedhi kuwa siri na kupelekea msichana kuwa na wigo awapo kwenye siku zake, mila hizo zisizuie wasichana na wanawake kujihakikishia hedhi salama yenye kumfanya mwanamke kuwa mwenye furaha wakati wote wa siku zake za hedhi.

Gudila Joakim mdau kutoka shirika la AceAfrica amefafanua kuwa, hedhi ni kitu cha kujivunia kwa mwanamke na huthibitisha kuwa mwanamkr aliyekamilika, na kutoa wito kwa watoto wa kiume kushirikiana vyema na watoto wa kike na sio kuwatenga pindi wanapopatwa na hali hiyo.

Maadhimisho ya siku ya hedhi yanafanyika kila tarehe 28.05 kila mwaka na mwaka huu yakiwa na kauli mbiu ya 'HAKUNA TENA KIKWAZO' yenye lengo la kuifanya jamii kushirikiana na kuhakikisha wanawake wanapata hedhi salama itakayomuwezesha kujisikia huru, mwenye furaha na mwenye kutekeleza majukumu yake bila kikwazo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.