• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ARUSHA DC YAANZA KUANDAA MAZINGIRA YA SHULE ZAKE, KUJIKINGA NA CORONA

Posted on: May 28th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

Halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, imeanza rasmi mchakato wa kuweka sawa mazingira ya shule zake tayari kwa  kukabiliana na kujikinga na gonjwa hatari la Corona, kwa kuanza kweka vifaa vya kunawia mokono katika shule zote za sekondari na msingi za halmashauri hiyo.

Imeelezwa kuwa, maandalizi hayo yameanza rasmi, kufuatia agizo la mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli,  kutangaza kuwa maambukizi ya ugonjwawa Corona yamepungua nchini na kuwataka wananchi kuendelea kufanyakazi huku wakijikinga na ugonjwa huo, kwa kuwa licha  ya ugonjwa huo kuwepo, maisha nayo lazima yaendelee.

Afisa Elimu Msingi, halmashauri ya Arusha, Hossein Mghewa, amekabidhi jumla ya ndoo 295 za kunawia mikono kwenye shule za serikali 95 za halmashauri hiyo na kuwataka walimu wakuu wa shule hizo, kufanya maandalizi ya kuhakikisha wanafunzi watasoma kwenye mazingira bora bila kupata maambukizi ya ugonjwa huo wa Corona pindi serikali itakapotangaza kufungua shule hizo.

Mghewa ameeleza kuwa vifaa hiviyo ni maandalizi, pindi serikali itakapotangaza shule kufunguliwa, kwa ajili ya kudhibiti na kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Corona unaosababishwa na Virusi vya Covid 19, na kuwataka walimu kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika ipasavyo kwa kufuata maelekezo ya watalamu wa afya.

"Tumejipanga kukabiliana  na ugonjwa wa Corona kwa kuhakikisha kila shule ina vifaa vya kunawia mikono, maji safi yanayotiririka na sabuni, ili wanafunzi waweze kunawa mikono mara kwa mara chini ya usimamizi wa walimu wao" amesema Afisa Elimu huyo.

Nao walimu wakuu licha ya kuishukuru serikali kwa kutoa vifaa hivyo shuleni, wameahidi kusimamia vema suala zima la kujikinga na ugonjwa wa Corona, kwa kusimamia ipasavyo maelekezo yote yanayotolewa na watalamu wa Afya na kuwaelekeza wanafunzi kufuata tabia chanya za usafi wao binafsi.

Katibu wa Walimu Wakuu na Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Emaoi, amesema kuwa, walimu wanapaswa kujiandaa kisaikolojia kuwa, wanakazi ya ziada ya kuhakikisha wanafunzi wanafuata taratibu zote za kujikinga na ugonjwa  wa Corona, kwa kuwadhibiti watoto kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni pindi shule zitakapokuwa zimefunguliwa.

"Ugonjwa upo, lazima tukabiliane nao, tunatakiwa kuwafundisha watoto namna ya kujikinga na maambukizi ya Corona, kwa nadharia na vitendo huku masomo yakiendelea" amesema Katibu huyo.

Halmashauri ya Arusha inaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo, kupambana na ugonjwa wa Corona, ugonjwa ambao hauna kinga wala tiba na umeenea kwa kasi duniani kote.


Afisa Elimu Msingi halmashauri ya Arusha, akimkabdhi ndoo za kunawia mikono1 Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Ngaramtoni, mwalimu Makanjo Twati tayari kwa maandalizi ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona pindi shule zitakapofunguliwa.


Baadhi ya Walimu Wakuu shule za Msingi, halmashauri ya Arusha wakiwa na ndoo za kunawia mikono kwa ajili ya shule zao, tayari kwa maandalizi ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona pindi shule zitakapofunguliwa.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.