• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU ATATUA MGOGORO WA MFEREJI WA MAJI KATI YA KIJIJI CHA MAJIMOTO NA WAMILIKI WA SHAMBA LA GOMBA ESTATE

Posted on: May 24th, 2023

DC ARUMERU ATATUA MGOGORO WA MFEREJI WA MAJI KATI YA KIJIJI CHA MAJIMOTO NA WAMILIKI WA  SHAMBA LA GOMBA ESTATE

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda ametatua mgogoro wa mfereji wa maji kati ya katika Kijiji cha Majimoto, kata ya Nduruma na Wamiliki wa shamba la Gomba Estate, mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka mitatu bila utatuzi.

Mgogoro huo ulikuwa unahusisha uongozi wa shamba la Gomba Estate kuzuia mfereji wa maji kupita katika shamba hilo kuelekea kwenye Kijiji cha Majimoto, mfereji ambao hutumika kwa shughuli za kilimo, hali iliyosababisha mazao ya wananchi hao kunyauka na kukosa mavuno kwa kipindi chote hicho.

Akizungumza na wananchi wa pande zote mbili kwa nyakati tofauti, Mhe. Emmanuela ameuagiza uongozi wa shamba hilo kuruhusu njia ya maji kupita katika shamba ili wananchi wa Majimoto waweze kupata maji na kunusuru mazao ya wananchi hao ambayo yananyauka shambani kutokana na ukame unaoendelea katika Kijiji hicho.

“Kaeni viongozi wa pande zote na kuweka kuweke utaratibu mzuri ili watu wote mpate maji kwa zamu, hairuhusiwi mtu yoyoyote kizuia maji kwa maslahi yake binafsi,  utaratibu wa zamu, utaratibu utakaowezesha kila upande kunufaika mtakao uweka kwa kuzingatia taratibu za Mamlaka ya Bonde la Mto Pangani wameshaweka utaratibu  na kutoa kibali cha kutumia maji haya”. Amesisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Hata hivyo, utatuzi huo umekuja baada ya wananchi wa Kijiji hicho cha Majimoto kutaka majibu kutoka kwa Serikali kuhusu mgogoro huo huku wakidai wamechoshwa na kero ya mazao yao kuharibika mashambani kwa kukosa maji ya uhakika na kusababisha kukumbwa na baa la njaa kwa kipindi chote hicho.

“Tunaamini viongozi wetu wanaohusika na maji wanafanya kazi zao vizuri, lakini huyu msimamizi wa shamba la Gomba Estate amekuwa chanzo cha mazao ya wanakijiji hiki kuungua kila mwaka”. Alisema mmoja wa wanakijiji hao, Yohana Ming’arana wakati akiwasilisha kero hiyo kwa Mkuu wa Wilaya.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia maji Bonde la Mto Nduruma, Mariaki Mollel ameahidi kuendelea kusimamia mgao wa maji hayo ipasavyo ili wananchi wote wa Kijiji hicho waweze kunufaika kwani hiyo ni Rasilimali ya Taifa na hakuna mwananchi yeyote mwenye umiliki wa maji huku akisisitiza upendo baina ya wanakijiji hao.

Awali wananchi wa kijiji cha cha Majimoto kata ya Nduruma kupitia Jumuia ya watumia maji, na Uongozi wa shamba la Gomba Estate waliingia kwenye mgogoro baada ya uongozi wa shamba hilo kuzuia mfereji wa maji kupita kwenye eneo la shamba la Gomba Estate.

"ARUSHA DC Ni Yetu, Tushiikiane Kuijenga"
#KaziIendelee







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.