• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AWATAKA WANAVIKUNDI KUHAKIKISHA WANAREJESHA FEDHA ZA MKOPO WANAZOPEWA

Posted on: February 3rd, 2023

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, amewataka wanawake kuhakikisha wanafanya miradi waliyokusudia ili kuweza kurejesha fedha hizo kwa wakati ili fedha hizo ziweze kuwanufaisha na wengine.

Mkuu huyo wa wilaya amesema hayo wakati wa hafla ya kukabidhi mkopo wa shilingi milioni 274 kwa vikundi  37 vya wanawake na vijana, hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya makao makuu ya halmashauri ya Arusha.

Mheshimiwa Emmanuela amewasiistiza wanavikundi hao kutambua fedha hizo zinatakiwa kurejeshwa baada tu ya kipindi cha neema, hivyo ni vema kutumia fedha hizo kwa kufanya miradi waliyoiandika kwenye maandiko yao na kuweza kurejesha kwa wakati.

"Tukirejesha fedha hizi kwa wakati tutatoa fursa ya kuwakopesha wengine na sisi wenyewe kukopeshwa kwa awamu nyingine, tumieni fedha hizi kwa nidhamu" Amesisitiza Mkuu huyo wa wilaya

Aidha amewasisitiza wanawake  kuwahamasisha na kuwaelimsiha vijana ili waweze kunufaika na mikopo isiyo na riba inayotolewa na serikali kupotia asilimi 10 za mapato ya ndani ya halmashauri

 "Kina mama tunalo jukumu la kuwaelimisha vijana wetu ili nao wajitokeze kwa wingi kuchukua mikopo hii, leo tunatoa mikopo lakini vikundi vya vijana ni viwili tu, ninaamini mikono ya kina mama inalea, waleeni vijana, wajengeeni uweo wa kufanya kazi kama ninyi ili wanufaike na fursa hii adhimu". Amesisitiza Mhe. Mkuu wa wilaya.

Hata hivyo wanavikundi waliopokea mikopo hiyo wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwapa fursa inayowawezesha kujikwamua kiuchumi, kupitia mikopo hiyo isiyo na riba.

Habibu Malia kijana mwenye ulemavu, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu kwa mpango huo wa kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi na kuwasihi vijana kujitokeza kutumia fursa hiyo, kwa kuwa ni kweli inapatikana.

"Tunaishukuru serikali yetu kwa kutupa mikopo hii yenye masharti nafuu, hata sisi vijana wa kijijini kabisa tumeweza kukopesheka, jambo ambalo halipatikani kwenye taasisi nyingine za kifedha". Amesema Joseph Mibaroi wa kikundi cha KIDALI Youth Group cha kata ya Mwandeti.

Akizungumza kabla ya kukabidhi mikopo hiyo, mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa kwa kipindi cha miaka 3 halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo ya shilingi bilioni 1.3 na kwa kipindi cha miezi sita ya mwaka wa fedha 2022/23 imekopesha shilingi milioni 509.

Naye Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Arumeru, Noel Severe ameipongeza halmashauri kwa kutekeleza Ilani ya chama ya mwaka 2020 - 2025 ya kupambana na umaskini kwa kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapa mikopo isiyokuwa na riba.

"Mikopo hii ni utekelezaji wa Ilani ya CCM, hivyo mnapaswa kuhakikisha mnaitumia vizuri iweze kuinua vipato vya familia pamoja na tunategemea mkapambane na kurejesha kwa wakati,,kulingana na utaratibu". Amesema Mwenyekiti wa CCM

Awali mkuu wa wilaya ya Arumeru amekabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 274 kwa vikundi vya wanawake na vijana ikiwa ni 10% ya mapato ya ndani  kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.


ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

KaziIendelee





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.