• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU: TUMEJIPANGA HAKUNA MTOTO WA ARUMERU ATAPOOZA KWA UGONJWA WA POLIO

Posted on: September 1st, 2022

Na Elinipa Lupembe

Kufuatia mkakati wa Serikali wa kutokomeza ugonjwa wa Polio nchini, wilaya ya Arumeru yenye halmashauri za Arusha na Meru, inatekeleza mkakati huo kwa kutoa chanjo ya Polio kwa watoto wa chini ya miaka 5, huku Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango akisisitiza, kuwa hakuna mtoto wa Arumeru atapooza kutokana na ugonjwa huo wa Polio.

Mkuu huyo wa wilaya amebainisha hilo, wakati akizindua kampeni ya chanjo ya Polio awamu ya tatu, inayohusisha watoto wa kuanzia umri wa miaka 0 - 5, uzinduzi uliofanyika katika Zahanati ya Lengijave halmashauri ya Arusha.

Mhandisi Ruyango amethibitisha kuwa halmashauri zote za wilaya ya Arumeru, zimefanya vizuri katika kuhakikisha watoto wa chini ya miaka 5, wamepata chanjo kwa awamu ya kwanza na ya pili, huku awamu hii ya tatu, wakiwa wamejipanga kufikia malengo waliyojiwekea ya kufikia watoto 145,219.

"Tumejipanga vema kuhakikisha  tunawafikia watoto wote wa chini ya miaka mitano na kuhakikisha wanapata chanjo ya Polio, lengo letu ni kuhakikisha hakuna mtoto wa Arumeru atapooza kwa ugonjwa huo, kwa kuwa mkakati wetu ni kuwapa chanjo watoto". Amesisitiza Mkuu huyo wa wilaya

Hata hivyo, uzinduzi huo ulipambwa na wanaume kuwaleta watoto kuoata chanjo, wakiwa kifua mbele kuhamasisha wanaume wenzao kushirikiana na wenza wao kuhudhuria Kliniki wakati wote wa ujauzito na watoto wa chini ya miaka mitano.

Joshua Samweli (28) baba wa mtoto Prisca Joshua mwenye umri wa mwezi (1), amesema kuwa yeye  huudhuria Kliniki na mwenza wake tangu wakati wote wa  ujauzito, lengo lake ni kufahamu maendeleo ya makuzi ya mtoto wake tangu akiwa tumboni, kuzaliwa mpaka kukua kwake.

Naye Julius Mathayo baba wa mtoto Gloria Losieku (1), amesema kuwa amelazimika kumpeleka mtoto wake kupata chanjo, ili kumkinga na ugonjwa wa Polio unaosababisha ulemavu wa kudumu na wakati  mwingine kifo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amethibitisha kutimiza maagizo ya mkuu wa wilaya kwa kuhakikisha watoto wote wanapatiwa chanjo ya Polio na kuongeza kuwa, halmashauri imejipanga kwa kuwa na vituo 59 vya kudumu vya kutolea huduma za Afya pamoja na pamoja na posti 201 zilizoandaliwa kwa ajili ya kutoa chanjo hizo wakati huu wa kampeni, kwenye ofisi za kata, vijiji na vitongoji.

Mganga mkuu halmashauri wa Arusha, Dkt. Petro Mboya, amekiri kuhakikisha wanadhibiti ugonjwa wa Polio kwa kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo zote dhidi ya ugonjwa wa Polio mara baada ya kuzaliwa na kukamilisha chanjo zote.

Aidha ameweka wazi kuwa, katika Kampeni ya Chanjo awamu ya (3), halmashauri hiyo inategemea kutoa chanjo dhidi ya Ugonjwa wa  Polio kwa watoto 88,628.

Ikumbukwe kuwa Kampeni ya Chanjo ya Polio yenye kauli mbiu ya Mpe chanjo, Okoa Maisha, inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na wafadhili wa  shirika la Watoto UNICEF pamoja na shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) lengo likiwa kuokoa maisha ya watoto.

Mpe Matone........, Okoa Maisha

ARUSHA DC

TUKO KAZINI✍

HAKIKISHA UMEHESABIWA


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA ZOEZI LA UZINDUZI WA KAMPENI YA CHANJO AWAMU YA 3 ZAHANATI YA LENGIJAVE

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango akimpatia mtoto Veronica Meru (miezi 3) matone ya chanjo ya Polio, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kampeni ya chanjo ya Polio awamu 3, halmashauri ya Arusha kwenye Zahanati ya Lengijave

Mkurugenzi Mtendaji  halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akimpatia mtoto Gloria Losieku (1) matone ya chanjo ya Polio, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya chanjo ya Polio awamu 3,  kwenye Zahanati ya Lengijave


Mganga mkuu halmashauri ya Arusha, Dkt. Petro Mboya, akimpatia mtoto Prisca Joshua (Miezi 3) matone ya chanjo ya Polio, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya chanjo ya Polio awamu 3,  kwenye Zahanati ya Lengijave


Wauguzi Halmashauri ya Arusha wakifurahia kumhudumia baba Julius Mathayo aliyeleta mtoto wake kupata chanjo ya Polio kwenye Zahanati ya Lengijave wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya chanjo ya Polio awamu 3,

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.