• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KATIKA  KUMBUKUMBU YA SIKU YA MASHUJAA NCHINI, JAMII IMETAKIWA KUITHAMNI NA KULINDA AMANI YA NCHI.

Posted on: July 25th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Jamii imetakiwa kuithamini na kuilinda amani ya Tanzania kwa kuwa amani na utulivu uliopo haipatikanini katika mataifa mengine na mataifa mengi wanaitamani na kuitafuta bila mafanikio.


Rai hiyo imetolewa na Kaim Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru, na Afisa Tarafaa kata ya Mbuguni, Abdala Teni, wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya siku ya mashujaa, yaliyofanyika kwenye shule mpya ya sekondari Kiutu, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.

Kaimu Katibu Tawala huyo, ameitaka jamii, kutambua kuwa misingi ya amani iliyopo nchini, imejengwa kwa muda mrefu na  mashujaa wazalendo wa nchi ya Tanzania, hivyo kila mtanzania ana jukumu la kuilinda tunu hii, ili iendelee kudumu vizazi hadi vizazi.

Kila mtanzania anapaswa kutambua kuwa, wapo mashujaa waliopambana na hata wengine kupoteza maisha kwa ajili ya kupambania ukombozi wa Taifa hili, wapo mashujaa walioingunisha Tanganyika na Zanzibar ambayo leo watanzania wanajivunia Muungano na kuongeza kuwa ili kuilinda amani hii ni lazima kuweka uzalendo mbele katika kuilinda amani ya nchi.

"Tunapowakumbuka mashujaa walioipigania na nchi yetu, kika mtanzania anapaswa kuiombea na kuilinda amani ya  Taifa hili ili iendelee kudumu, tunapaswa kuulinda Muungano kwa nguvu zote, tusikubali kupoteza amani yetu kwa itikadi za dini, siasa wala makabila kwa kuwa wapo mashujaa walioijenga misingi imara ya amani na utulivu wa Taifa la Tanzania" Amesisitiza Teni.


Naye Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, ameeleza licha ya kuwa lengo la kumbukizi ya siku hiyo, ni kuwakumbuka mashujaa waliopambania ukombozi wa nchi yetu, lakini zaidi ni kuendelea kuyaenzi matunda ya kuipigania nchi hii kwa kudumisha amani, upendo na mshikamano.


"Serikali inatambua na kuthamini damu ya watanzania iliyomwagika kwa ajili ya ukombozi wa nchi ya Tanzani, ni vema watanzania kwa umoja wetu, kudumisha amani iliyopo bila kujali tofauti zetu za kidini, kisisasa wala makabila yetu, Tanzania ni moja " amesisitiza Msumi.


Hata hivyo katika maadhimisho hayo, kulihudhuriwa na mzee shujaa wa Tanzanzia,  ambaye ni mwenyekiti wa CCM kata ya Kiutu, mzee Wilson Meiludie, ambaye alishiriki vita vya Kagera na Uganda, mwaka 1978-79, amewataka watanzania kudumisha amani kwa kuwa madhara ya vita ni makubwa kwa jamii, madhara ambayo huacha makovu makubwa kwenye mioyo ya wanadamu.

"Niwasihi ndugu zangu, msiombe vita katika nchi yetu, nimeishuhudia vita, ni kitu ambacho sio kizuri kutokea katika jamii, watu wasio na hatia hupoteza maisha, huku uchumi wa nchi husika ukiporomoka na ni vigumu sana kuirudisha amani iliyopotea kwa ajli ya vita, tuna mifano kwa nchi za jirani, kwa miaka mingi wanapambana kuiridusha amani bila mafanikio" amebainisha mzee Meiludie

Awali wananchi halmasahuri ya Arusha, wameungana na watanzania kuadhimisha kumbukumbu ya siku ya Mashujaa nchini kwa kufanya usafi wa mazingira pamoja na kuotesha miti katika shule mpya ya sekondari Kiutu kata ya Kiutu.

Maadhimisho ya kumbukumbu ya siku mashujaa, yamefanyika kitaifa jijini Dodoma na hufanyika tarehe 25 Julai kila mwaka.

ARUSHA DC

#KaziInaendelea

JIANDAE KUHESABIWA


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA SIKU YA MASHUJAA 2022


Kaim Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru, na Afisa Tarafaa kata ya Mbuguni, Abdala Teni, akiotesha mti kwenye shule mpya ya sekondari Kiutu, ikiwa ni shughuli za maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku ya Mashujaa.



Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akiotesha mti kwenye shule mpya ya sekondari Kiutu, ikiwa ni shughuli za maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku ya Mashujaa.


Mmoja wa mashujaa wa Tanzania, Mzee Wilson Meiludie, aliyeshiriki vita ya Uganda na Kagera, akiotesha mti kwenye shule mpya ya sekondari Kiutu, ikiwa ni shughuli za maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku ya Mashujaa.


Mwenyekiti Halmashauri ya Arusha Mhe. Ojung'u Salekwa, akiotesha mti kwenye shule mpya ya sekondari Kiutu, ikiwa ni shughuli za maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku ya Mashujaa.






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.