• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KUELEKEA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA, WAZAZI ARUSHA, WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO YA MALEZI KWA WATOTO WAO

Posted on: June 13th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2022, mkoa wa Arusha, umejipanga kuendelea kupambana na ukatili dhidi ya watoto kwa kuwataka wazazi na walezi kuacha kukwepa majukumu yao ya malezi kwa watoto wao, jambo ambalo linasababisha watoto kufanyiwa vitendo vya ukatili ndani ya familia zao.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo ya siku moja, yaliyojumuisha waandishi wa habari, watoto, watalam na wadau, Katibu Tawala mkoa wa Arusha, Dkt. Athman Kihamia, ameweka wazi kuwa mkoa wa Arusha, umeweka mikakati ikiwemo kuelekeza nguvu katika kuimarisha juhudi za kumlinda mtoto wa mkoa wa Arusha dhidi ya ukatili na hatimaye kutokomeza ukatili mkoani humo huku akiwataka wazazi kuwa karibu na watoto wao, licha ya changamoto za utafutaji wa riziki na vipato vya familia.

Licha ya kuwa serikali ina mikakati imara ya kupambana na ukatili dhidi ya watoto, zaidi amewataka wazazi na walezi kutekeleza majukumu yao ya malezi kwa kuwasimamia watoto na si kuwaachia walimu ama wasaidizi wao wa nyumbani, kulea watoto wao, jambo ambalo limekuwa ni sababu ya watoto wengi kufanyiwa ukatili bila wazazi kufahamu kwa kuwa wanawaamini watu hao.

Amefafanua kuwa jukumu la malezi ya watoto ni wazazi, lakini wazazi wamejikita zaidi kufanya kazi kwa ajili ya kujipatia kipato na kuacha jukumu la malezi kwa walimu na wasaidizi wa ndani jambo ambalo linasababisha watoto kufanyiwa vitendo vya ukatili ndani ya nyumba zao.

"Matukio mengi ya ukatili yanafanyika ndani ya familia zetu na ndugu wa karibu tunaowaamini, kama wazazi watatimiza wajibu wao wa kulea watoto, watoto watakuwa katika maadili mema na matukio ya ukatili yatapungua, na hatimaye kuwa na jamii yenye maadili mema, lakini wazazi wamekuwa chanzo cha watoto kufanyiwa ukatili majumbani" amesisitiza Katibu Tawala huyo.

Naye Inspekta Happy Mshana, kutoka Dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Arusha, amekiri kuwepo na uzembe mkubwa unaofanya na wazazi katika malezi ya watoto, kwani asilimia kubwa ya wazazi hawawafamu vizuri watoto wao, kutokana na muda mwingi kuwaachia walimu, wasaidizi wa kazi ama ndugu wanaoishi nao nyumbani, miongoni mwao ndio wanawafanyia watoto ukatili huku akiwalaumu baadhi ya wazazi kuwasaidia wahalifu wa ukatili kutoroka kwa kufanya nao maridhiano nyumbani.

"Katika kesi za watoto tunazozipokea, wazazi wengi hawajui tabia za watoto wao, kutokana na ubizy wa kuoambana na maisha, ukikaa na watoto wanaeleza mambo ambayo hata wazazi wao hawayajui, na ukiwapeleleza kwa undani, wanasema sisi tunabaki na dada, anko au mamdogo,  jambo ambalo linatoa mwanya kwa watoto kufanyiwa vitendo vya ukatili, niwatake wazazi kuwa karibu na watoto wao, ili kuwajua vema na kufahamu changamoto zizowakabili" amesisitiza Inspekta Happy.

Hata hivyo, watoto kutoka shule za tofauti za mkoa wa Arusha, wameishukuru serikali kupitia wimbo maalumu kwa kuanzisha Dawati la Jinsia na Watoto, Dawati ambalo limewezesha kutatua changamoto za watoto wanaofanyiwa ukatili, huku baadhi ya watoto  wakipata wakipata haki zao, na watuhumiwa kuhukumiwa kutokana na makosa yao.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kupitia kitengo cha Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na wadau wa shirika la DSW, CWCD na SOS Children Village, wameandaa, mafunzi ya siku moja yaliyojumuisha waandishi wa habari, watalamu, watoto na wadau, ikiwa ni maandalizi ya maadhimisho ya Siku  ya  Mtoto wa Afrika yenye  kauli mbiu "Tuimarishe ulinzi wa mtoto; Tokomeza Ukatili Dhidi yake: Jiandae Kuhesabiwa"


#KaziIendelee✍✍


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MAFUNZO 

Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Dkt. Athman Kihamia, akizungumza wakati wa kufungua mafunzo juu ya mapambano ukatili dhidi ya watoto, mafunzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha.

 

Watoto wakifuatilia mada zilizokuwa zinatolewa wakati wa mafunzi ya mapambano ya ukatili dhisi ya watoto, kwenye ukumbi wa Ofisi ya MKuu wa mkoa wa Arusha.


Inspekta Happy Mshana, kutoka Dawati la Jinsia na Watoto, mkoa wa Arusha, akifuatilia mada zilizotolewa juu ya mapambano ya ukatili dhidi ya watoto, kwenye ukumbi wa mikutano, ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha.








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.