• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAKAMU WA RAIS, AZINDUA MAJENGO YA CHUO CHA MISITU OLMOTONY

Posted on: November 8th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa, Samia Suluhu Hassan, ameipongeza serikali ya Norway kupitia Ubalozi wa Ufalme wa nchi hiyo,  nchini Tanzania,  kwa kufadhili ujenzi wa miundombinu katika Chuo cha Misitu Olmotony,halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru.

Makamu wa Rais, ametoa pongezi hizo, mapema leo,  wakati akizindua jengo la mihadhara na bweni la wanafunzi, katika Chuo cha Misitu Olmotony, na kuipongeza Serika kifalme ya Norway kwa kwa juhudi zake za kufadhili Taasisi za Elimu ya Uhifadhi wa Misitu na Mazingira.

Katika hafla hiyo, Makamu wa Rais amezindua jengo la mihadhara lenye uwezo wa uwezo wa kusomesha wanafunzi takribani  240, pamoja na Bweni la wanafunzi wa kike lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 100, majengo yaliyogharimu kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 1.8, ujenzi uliofadhiliwa na Serikali ya Kifalme ya Norway kupitia Mradi wa Kujenga uwezo wa Jamii kwa njia ya mafunzo katika Usimamizi Shirikishi wa Misitu, MKUHUMI na Mabadiliko ya Tabianchi maarufu kama ECOPRC.

Makamu huyo wa Rais, amesema kuwa, majengo ni muhimu sana kwa chuo hicho, kwa kuwa yatasaidia kupunguza uhaba wa madarasa uliokuwepo, pamoja na kuimarisha ustawi wa wanafunzi wa kike licha ya waondolea adha ya kupanga nyumba za watu binafsi nje ya chuo.

Aidha Mhe, Samia ameendelea kuushukuru Ubalozi huo  kwa  kutoa ufadhili kwa wanafunzi 128 kimasomo katika ngazi ya Astashahada na Stashahada, chuonini hapo huku wanafunzi 56 kati yao wakiwa ni wanawake.

Zaidi Mhe Samia ameushukuru mambo mengi, yaliyofanywa na  Ubalozi huo  ikiwa ni pamoja na kukiunganisha chuo hicho kwenye Mkongo wa Taifa, kuboresha maktaba  pamoja na kukiwezesha kununua vifaa mbalimbali kwa ajili ya  kufundishia.

Ameongeza kuwa, juhudi zote hizo zitasaidia kuimarisha mazingira ya kujifunzia, pamoja na kutoa taaluma bora, itakayowezesha kuzalisha watalaam wenye ujuzi wa kiwango cha hali ya  juu.

Hata hivyo Makamu wa Rais, ameelezea changamoto ya ukataji miti hovyo na uzembe katika upandaji miti zinavyoharibu uoto wa asili na kusababisha uharibifu na mazingira ya asili, na kuzitaka taasisi husika kusimamia, kusimamia upandaji na utnzaji wa miti pamoja na kuwa na takwimu sahihi za idadi ya miti.

Awali, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga, alieleza kuwa kutokana na uhaba wa mabweni na kumbi za mihadhara, Chuo kilikuwa na uwezo wa kudahili wanafunzi wachache kulingana na mahitaji, kwa kudahili wanafunzi 600 tu badala ya kudahili wanafunzi zaidi ya 1,000.

Mhe, Hasunga amesema kuwa licha ya ujenzi wa miundombinu hiyo kusaidia kuboresha utoaji wa mafunzi ya kiwango cha juu lakini pia utawezesha chuo hicho kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa.

Aidha, Naibu Waziri Hasunga, ameuomba  Ufalme wa Norway kuendelea kushirikiana na Chuo hicho, ikiwemo kuendelea kuongeza mabweni ya wavulana, madarasa pamoja na kuboresha vifaa vya mafunzo ili chuo kiweze kufikia lengo lake la kuongeza udahili wa wanafunzi chuonj hapo.

Naye Balozi wa Norway nchini, Elizabeth Jacobsen amesema kuwa, lengo la nchi yake kufadhili  mradi huo, ni kuimarisha ustawi wa miti na kuhakikisha, miti iliyopo haikatwi ovyo badala yake jamii ijikite zaidi katika kupanda miti, ili kuepuka majanga yanayotokana na mabadiliko ya tabianchi.

Chuo cha Misitu-Olmotonyi  kilianzishwa mwaka 1937, kwa madhumuni ya kufundisha elimu ya uhifadhi wa misitu kwa ngazi ya ufundi-sanifu na  kimekuwa tegemeo kubwa ndani na nje ya Tanzania, hasa katika ukanda wa Kusini mwa Afrika.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.