• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Milioni 296.4 za TASAF zatekekeleza miradi ya Elimu na Afya Arusha DC

Posted on: October 22nd, 2018

Zaidi ya shilingi milioni 296.4 za TASAF  zimeanza kutekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu kwenye sekta ya Elimu na Afya katika kata za Bangata, Sambasha na Bwani, halmashauri ya Arusha wilayani Arumeru.

Miradi hiyo kwa pamoja, inategemea kukamilika katika mwaka huu wa fedha wa 2018/19 na kuanza kutoa huduma kwa wananchi wa maeneo hayo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mratibu wa TASAF wa halmashauri ya Arusha, Grace Makema, amesema kuwa, kiasi hicho cha fedha kinatumika kutekeleza jumla ya miradi minne katika sekta ya elimu na afya.

Amefafanua kuwa katika miradi ya elimu jumla ya shilingi milioni 194.4 zimetumika kwenye ujenzi wa nyumba mbili za walimu zenye sehemu mbili (2in 1) katika  shule ya msingi Mungushi kata ya Bwawani, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, ofisi ya walimu na vyoo shule ya sekondari Sambasha pamoja ujenzi wa nyumba ya walimu shule ya msingi Engikaret kata ya Bangata.

Aidha ameitaja gharama za  kila mradi na kufafanua kuwa, ujenzi wa vyumba vya madarasa na choo chenye matundu sita,  shule ya Sekondari Sambasha umegharimu kiasi cha  shilingi milioni 74.3, na nyumba ya walimu Engikarate shilingi milioni 50 na nyumba ya walimu shule msingi Mungushi umegharimu kiasi cha shilingi milioni 70.

Makema ameutaja mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Midawe katika kata ya Bangata, mradi unaogarimu zaidi ya shilingi milioni 102.

Hata hivyo Mratibu huyo, amethibitisha kuwa, chanzo cha miradi hiyo ni wananchi wa maeneo husika ambao waliibua miradi hiyo kutokana na vipaumbele vyao na baadaye kupitishwa kwenye mikutano mikuu ya vijiji kwa makubaliano ya wananchi, ambayo ilifanyika katika  mwaka wa fedha 2016/2017 na ikaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha wa 2017/2018.

Pia amebainisha kuwa lengo la TASAF kutekeleza miradi hiyo ni kuwapunguzia wananchi mzigo wa kuchangia fedha kwaajili ya kugharamia ujenzi wa miundombinu ya kutolea huduma za jamii pamoja na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi.

“ TASAF iliamua kutekeleza miradi hiyo yote katika maeneo hayo baada ya kuthibitisha kuwa kuna uhitaji wa miradi hiyo kutekelezwa katika maeneo hayo, ili kuwawezssha wananchi kupata huduma kwa urahisi" amesema Mratibu huyo

Kwa upande wake, mjumbe wa serikali ya kijiji cha Sambasha, Samweli Kwesam, ameishukuru serikali kupitia miradi yake ya TASAF kwa kutekeleza mradi wa madarasa na vyoo katika shule ya sambasha,  ambao kwa kiasi kikubwa umewasaidia wananchi kuepuka kuchangia garama kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo.

Aidha amesema kuwa, shule hiyo ilikuwa na uhaba mkubwa wa vyumba vya madarasa kutokana na shule hiyo kuwa ni changa na wananchi walianza kuchangishana na kujenga chumba kimoja cha darasa lakini kutokana na juhudi za serikali, hadi sasa shule hiyo ina jumla ya vyumba kumi vya madarasa  ambayo mawili kati ya hayo yamejengwa na TASAF na kutosheleza wanafunzi wote..

“Kama wananchi wa Sambasha, tuliithamini elimu na mwaka 2014 wananchi tulishirikiana na viongozi wetu na kuamua kujenga, jengo moja ambalo mwaka 2015 wanafunzi walianza kusoma lakini mpaka sasa hivi tuna majengo kumi pamoja na maabara tatu za kisasa”alisema Kwesam.

TASAF awamu ya III inatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo, miradi ya ujenzi, miradi ya mazingira, mifugo, kilimo pamoja na mradi wa uhawilishaji fedha kwa kaya masikini.


Vyumba vya madarasa na ofisi ya walimu, shule ya sekondari Sambasha kata ya sambasha.


Nyumba ya walimu yenye sehemu mbili  (2 in 1)shule ya msingi Mungushi kata ya Bwawani.

Nyumba ya walimu yenye sehemu mbili (2 in 1) shule ya Msingi Engikaret kata ya Bangata.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.