Na Elinipa Lupembe.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung' u Salekwa na familia yake, tayari ametimiza wajibu wake, kama Mkuu wa Kaya, kwa kuhesabiwa kwenye Sensa ya Watu na Makazi nyumbani kwake kijiji cha Enjoro kata ya Laroi.
Mwenyekiti Ojung'u ameipongeza serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuandaa mpango wa Sensa ya watu na makazi, zoezi ambalo litaiwezesha serikali kupanga mipango bora kulingana na takwimu za idadi ya watu zitakazopatikana.
"Sensa ni muhimu sana kwa mipango ya serikali makini, takwimu za Sensa zitaiwezesha serikali kupanga mipango kulingana na idadi ya watu na mahitaji yao kisekta kulingana na makundi yao".Amesema Mwenyekiti Ojung'u.
Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewasihi wananchi kujitoa ushirikiano kwa makarani wa Sensa watakaofika kwenye kaya zao na kutaka taarifa zinazohitajika kwenye dodoso la Sensa huku akiwataka kaya zenye watu wenye ulemavu kuhakikisha nao wamehesabiwa ili serikali iweze kupanga mipango bora kwa ajli yao.
Zoezi la Sensa ya watu na Makazi linaendelea katika halmashauri ya Arusha,huku kukiwa na hali ya amani na utulivu, wakazi wa halmasahuri hiyo wakiwa nyumbani kusubiri Makarani wa Sensa kufika kwenye kaya zao.
HAKIKISHA UMEHESABIWA✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.