• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI KUPITIA TASAF YAWEZESHA UJENZI WA ZAHANATI MPYA KIJIJI CHA ENGUTUKOIT

Posted on: March 21st, 2023

Na Elinipa Lupembe

Serikali ya awamu ya sita kupitia Mfuko wa Maendleeo ya Jamii (TASAF)  imefanikisha  ujenzi wa Zahanati mpya Kijiji cha Engutukoit  Kata ya Oldonyowas Halmashauri ya Arusha kwa gharama ya shilingi milioni 102.


Ujenzi wa zahanati hiyo, umefanyika kufuatia mkakati wa Serikali  ya kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ili kukabiliana na vifo vya wanawake na watoto.


Ujenzi wa zahanati hiyo, utasaidia kuokoa maisha ya wakazi wa kijiji hicho hususani kina mama wajawazito na watoto ambao hapo awali walitembea umbali mrefu kutafuta huduma za Afya huku baadhi yao wakipoteza maisha kwa kukosa huduma za haraka.


Wakizungumzia kwa  hisia  baadhi ya wakazi wa Engutukoit wakati ujenzi wa zahanati ukiendelea,

wamesema kuwa, zahanati hiyo itakuwa ni mkombozi wa akina mama wajawazito kujifungulia sehemu salama badala ya kujifungulia nyumbani kama ilivyokuwa hapo awali.


Wamesema kuwa, wajawazito walilazimika kujifungulia nyumbani jambo ambalo lilihatarisha maisha yao na watoto, huku watoto wa chini ya miaka 5 wakishindwa kuhudhuria kliniki kwa usahihi kutokana na kushindwa kumudu gharama za usafiri kwa kila mwezi.


“Tulikuwa tunapata shida sana endapo ikitokea dharura ya mgonjwa nyakati za usiku, ilitulazimu  kukodi pikipiki kwa shilingi elfu 30 kumpeleka mgojwa kupata matibabu kwenye kata jirani ya Oldonyosambu, lakini sasa tunafurahi kwa kuwa tutapata huduma za afya hapa karibu na nyumbani.” Ameweka wazi Jackline Saruni.


Hata hivyo wananchi hao wameishukuru sana Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia TASAF kwa kuwakumbuka na kuwajengea zahanati hiyo kwani walikaa miaka mingi bila kupata huduma hiyo muhimu katika kijiji chao.


"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.