• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali yaanza ujenzi wa Maktaba shule za sekondari za kata

Posted on: April 6th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.


Kufuatia sera ya Serikali ya awamu ya tano ya kutoa elimu bila malipo, kuanzia shule ya awali mpaka kidato cha nne, sera inayoenda sambamba na mkakati thabiti wa uboreshaji wa miundombinu ya shule, kupitia miradi yake ya Lipa kutokana na Matokeo 'EP4R', imeanza kujenga maktaba kwenye shule za sekondari za kata nchini.


Halmashauri ya Arusha,  ni miongoni mwa halmashauri zilizonufaika na neema hiyo,  kwa kupewa kiasi cha shilingi milioni 100, kwa ajili ya ujenzi wa maktaba katika shule zake mbili za sekondari za Mwandet na Mlangarini.


Akizungumzia adhma ya serikali ya awamu ya tano, Mkurugenzi mtendaji, halmashauri hiyo, Dkt. Wilson Mahera, amesema kuwa, katika kuboresha miundombinu ya shule, serikali imekwenda mbali zaidi kwa kuanza kujenga maktaba kwenye shule za sekondari za kata, ambazo hapo awali shule hizo hazikuwa na maktaba.


Amesema kuwa, maktaba ni sehemu muhimu katika mchakato mzima wa ufundishaji na kujifunza, unaompa fursa mwanafunzi kujisomea zaidi akiwa mwenyewe na kujipatia maarifa zaidi, kwa yale aliyofundishwa na mwalimu akiwa darasani.


"Maktaba ni muhimu katika shule, inakuza taaluma na inamfanya mwanafunzi kujisomea kwa uhuru na kupata maarifa katika mawanda mapana zaidi,  kwa kile alichofundishwa na mwalimu darasani, pamoja na kujifunza mambo mbalimbali ya kijamii" amesema mkurugenzi huyo


Wadau mbalimbali wa elimu wametoa maoni yao tofauti juu ya umuhimu wa ujenzi huo makta kwenye shule za kata, licha  ya kuipongeza na kuishukuru serikali ya awamu ya tano, kwa kuwekeza fedha nyingi kwenye kuboresha miundombinu ya elimu, kutokana na ukweli kwamba mazingira bora ya kujifunzia,  ni chachu ya mwanafunzi kujifunza  na kumwezesha mwanafunzi kuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa kile alichofundishwa.


Janeth Shayo mwalimu wa shule ya msingi Olchoki, halmashauri ya Arusha, amethibitisha kuwa, kuna tofauti kubwa ya kujifunza kati ya mwanafunzi aliye kwenye mazingira bora na vifaa, na yule anayejifunza kwenye mazingira duni yasiyo na vifaa.


Ameongeza kuwa  uwepo wa mazingira bora na vifaa vya kujifunzia,  hutoa msukumo chanya kwa mwanafunzi kujifunza tofauti na  yule aliye kwenye mazingira duni kwani huwa na msukumo hafifu na wakati mwingine huwa hasi kabisa.


Naye mkuu wa shule ya sekondari  Mlangarini, mwalimu Elisa Pallangyo, ameshukuru na kupongeza juhudi za serikali, za kuwekeza hasa kwenye shule changa, shule za kata ambazo zimeanza huku zikiwa,  hazijitoshelezi hasa katika miundombinu yake.


Amesema kuwa, uwepo wa maktaba shuleni kwake, utawawezesha wanafunzi kuwa na muda wa kutosha wa kujisomea, na kwa  utulivu zaidi  kuliko wawapo madarasani, huku maktaba hiyo ikisaidia utunzaji rahisi na imara  wa vitabu, tofauti na hapo awali ambapo kulikuwa na upotevu wa vitabu.


" Maktaba itawawezesha wanafunzi kupata muda zaidi wa kujisomea wenyewe na kwa utulivu, pamoja na urahisi wa upatikanaji wa vitabu unaoenda samvamba na utunzaji wa vitabu, ambao kwa sasa ni mgumu, kw kuwa vitabu vinapotea kwa urahisi" amesema mkuu huyo wa shule.


Aidha, ujenzi wa maktaba zote mbili uko kwenye hatua za boma huku ukiendelea kwa kasi na unategemewa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu wa Aprili na wanafunzi kuanza kupata huduma bora kwenye majengo hayo yote.


Awali, Halmashauri ya Arusha imepokea kiasi cha shilingi milioni 220, kutoka serikali kuu kupitia wizara ya Elimu na miradi ya EP4R, fedha ambazo milioni 110, zimetumika kujenga maktaba katika shule ya sekondari Mwandet na Mlangarini, kwa gharama ya shilingi milioni 50 kila mmoja, huku shilingi milioni 110 zikitumika kukarabati na kumalizia mabwalo ya chakula kwa shule zote mbili.


PICHA ZA MAJENGO YA MAKTABA HIZO


Muonekano wa jengo la Maktaba shule ya sekondari Mlangarini.



Muonekano wa jengo la Maktaba ya shule ya sekondari Mwandeti.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.