• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA CWCD KUANZISHA KLABU ZA KUZUIA UKATILI DHIDI YA WATOTO KWENYE SHULE 30 ARUSHA DC

Posted on: August 3rd, 2019

Kufuatia mpango mkakati wa Serikali ya awamu ya tano, wa kupambana na kuzuia ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini, halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, imejipanga kuanzisha klabu  za watoto kwenye shule zake 20 za msingi na sekondari, kwa mwaka huu wa fedha 2019/2020.

Mkakati huo umewekwa wazi wakati wa mafunzo ya ufunguzi wa mradi huo, unaotegemea kutekelezwa na shirika la Center for Women and Children Development 'CWCD', kwa ufadhili wa shirika la Civil Society Foundation, uliowakutanisha watalamu wa halmashauri kuanzia ngazi ya kijiji, viongozi wa serikali na wawakilishi wa wananchi ikiwemo madiwani na wenyeviti wa vijiji na vitongoji, mafunzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Mwezeshaji wa Mafunzo kutoka shirika la CWCD, Happy Josephat, amesema lengo la mradi huo kuanzisha klabu shuleni ni kuzuia ukatili dhidi ya watoto, kwa kuwajengea watoto uwezo wa kujitambua, kutambua haki na wajibu wao, kufahamu jukumu lao la kujilinda dhidi ya ukatili na uwezo wa kutoa taarifa kwa wakati.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajenga, uelewa wa pamoja kwa watalamu na viongozi wa jamii ili kushirikiana kwa pamoja kupambana na ukatili dhidi ya watoto.

Aidha ameeleza  kuwa, shirika linajukumu la kuwajengea uwezo walimu, watakaowafundisha watoto hao, kwa usimamizi wa viongozi wote wa serikali na jamii ili kupambana na ukatili dhidi ya watoto.

Naye Mkurugenzi Mtendajim halmashauri ya Arusha, licha ya kulishukuru shirika hilo, ameahidi kutoa ushirikiano na kuwataka watalamu wa ngazi za kata na vijiji pamoja na walimu, kutumia fursa hiyo kuzuia ukatili wa watoto katika maeneo yao.

Ameongeza kuwa licha ya matukio hayo, kuanza kupungua kwa sasa, lakini bado kuna maeneo ambayo yanachangamoto, zinazotokana na mila na desturi, na kuitaka jamii kubadilika na kutokomeza mila hizo, zinazowadhalilisha watoto na wanawake kwa kuwakandamiza na kuwanyima haki zao za msingi.

Hata hivyo, viongozi walioshiriki mafunzo hayo, wamelalamikia mahakama na polisi, kushindwa kutoa haki kwa watoto waathirika wa ukatili na badala yake, watuhumiwa kuachiwa huru kwa madai ya kukosa ushahidi, na kuwaacha viongozi uhasama na familia za watuhumiwa.

Diwani wa kata ya Kiranyi, mheshimiwa Jombi Seneu, amethibitisha kuwa, viongozi wanajitahidi kupambana na ukatili katika maeneo yao, na kuwakamata watu wanaofanya vitendo, hivyo lakini bado sheria za polisi na mahaka zinapaswa kuangaliwa upya, kwa kuwapa nafasi watuhumiwa kudhaminiwa na kumaliza kesi hizo kwa mazungumzo mezani, matokeo yake viongozi na watu walioshiriki kumkamta mtuhumiwa kubaki na uhasama na familia ya mtuhumiwa.

"Viongozi na wananchi,tunamkamata mtuhumiwa na kumfikisha polisi, polisi anapewa dhamana, anakuja nyumbani anapata nafasi ya kukaa na ile familia wanazungumza, bado sheria ni kinzani, zinazopoteza au kuharibu ushahidi, pindi mtoto anapofanyiwa ukatili, zinapaswa kuangaliwa upya" amesema Diwani Seneu.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, jamii imeelekeza lawama kwa wazazi, kwa madai kuwa licha ya juhudi za serikali, wadau, viongozi na jamii kunia mamoja, bado wazazi wako nyuma katika mapa,bano ya kutokomeza ukatili dhidi ya watoto, kwa kukubali kumalizana na watuhumiwa, kwa  kushiriki kuficha watuhumiwa wanaowapa mimba watoto wa kike, kuwaozesha watoto, kuwafanyia tohara watoto wa kike, kuficha siri za matukio ya ubakaji na ulawiti yanayofanyika ndani ya familia zao.

Hindu Mbwego, mkurugenzi wa shirika la CWCD amethibitisha kuwa, bado wazazi wameshindwa kutekeleza majukumu yao katika kutokomeza ukatili dhidi ya watoto, licha ya serikali na jamii kuungana tupambana na wahalifu wanafanya vitendo vya ukatili kwa watoto.

Amefafanua kuwa, jamii inamkamata mtuhumiwa na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, kukiwa na yshahidi wa kutosha, lakini wazazi wanakubali kuzungumza na mtuhumiwa, matokeo yake wanamfundisha mtoto kubadilisha ushahidi, pengine wanamuhamisha na wakati mwingine kumzuia au kutokumpeleka mtoto mahakamani wakati wa kesi.

Hata hivyo Hindu ameeleza kuwa, matukio mengi ya ukatili kwa watoto yanafanyika nyumbani ndani ya familia, hivyo watuhumiwa wengi ni ndugu na jamaa, hivyo wazazi kushindwa kusimamia wajibu wao kwa kumtetea mtoto na badala yake, husimamia mahusiano yao na watuhumiwa ndani ya familia zao.

" Wazazi wanashirikiana na watuhumiwa, ama kwa kupewa fedha au kwa kuwa watuhumiwa ni member wa familia, pengine ni baba, mjomba ama babu, wazazi wanashindwa kusimama kumtetea mtoto wao kwa kuwakinga ndugu na jamaa zao na kuhofia kujenga uhasama kwa ndugu zao."

Awali mradi huo wa mwaka mmoja unategememea kutekelezwa kwenye shule 30 kwenye kata za Bangata, Ilboru, Kiranyi, Moivo, Oloirien, Olturoto na Tarakwa, ikiwa shule 20 za msingi na 10 za Serikali.












Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.