Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala zaMikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wote nchini kuhakikisha wanashughulikia changamoto za Halmashauri ingali mapema kuliko kusubiria mpaka Tumeziunde kuja kuchunguza.
Bashungwa ameyasema hayo wakati akifunga Kikao kazi za Wakuu wa Mikoa cha kuwapitisha kwenye Sura ya Mipango na Bajeti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa mwaka wa fedha 2022/23.
Amesema ninyi ni wasimamizi wa Halmashauri kwenye Mikoa yenu ikiwa mambo hayaendi sawa katika eneo lolote ni rahisi kujua mapema sasa kwanini msidhibiti changamoto hizo mnasubiria mpaka TAMISEMI tulete Tume wakati uwezo na Mamlaka mnayo? Alihoji Mhe. Bashungwa
Sasa nataka kuona mnachukua hatiamapema kabla mambo hayajaharibika huko hii itasaidia kupunguza malalamiko na shughuli za maendeleo kutekelezwa kwa ubora.
Halikadhalika Mhe. Bashungwa ameelekeza viongozi hao kusimamia ipasavyo Mfumo wa Nidhamu ya Watumishi katika Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kushughulikia watumishi wote wanaokwenda kinyume na sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.
Mhe. Bashungwa alihitimisha kikao hicho kwa kuwataka viongozi hao kuendelea lkuongeza usimamizi kwenye Ukusanyaji waMapato ya ndani ya Halmashauri ili kufikia Malengo ya kukusanya zaidi ya shilingi Trilioni moja kwa mwaka wa fedha wa 2022/23.
Chanzo: TAMISEMI
KaziIendelee✍✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.