• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF YAMWAGA MILIONI 216. 98 KUTEKELEZA MIRADI MITATU ARUSHA DC

Posted on: November 1st, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF, umeendelea kuimarisha, maisha ya wakazi wa halmashauri ya Arusha kisekta, tangu TASAF awamu ya III kupitia miradi ya  OPEC, ilipoanza kutekelezwa mwezi Juni mwaka 2013.

Wananchi wa halmashauri hiyo, wameemdelea kunufaika katika sekta za Elimu, Afya, Kilimo na Mifugo, miundombinu ya barabara, uwezeshaji wananchi kiuchumi, huku kaya masikini zikiendelea kupokea fedha za ruzuku, kupitia utekelezaji wa mradi wa Uhawilishaji fedha kwa Kaya Masikini.

Kwa kipindi cha robo ya pili, ya mwaka huu wa fedha 2019/2020, halmashauri ya Arusha, imepokea kiasi cha shilingi milioni 216.98, kwa ajili ya kutekeleza miradi mitatu, katika sekta ya Elimu na Miundombinu ya barabara.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Alvera Ndabagoye, amethibitisha halmashauri yake, kupokea kiasi hicho cha fedha, kilichoelekezwa kutekeleza miradi mitatu, ikiwemo ujenzi wa Kivuko cha Laroi kata ya Laroi, ujenzi wa nyumba mbili za walimu zenye sehemu mbili (2 in1), nyumba zenye uwezo wa kuishi  familia mbili kwa kila nyumba, kwenye shule ya msingi Lemuguru kata ya Matevesi na shule ya msingi Losikito kata ya Mwandeti.

Aidha mkurugenzi Alvera, amefafanua kuwa, halmashauri imejipanga vema kutekeleza miradi hiyo kwa wakati, na hasa kwa kuzingatia ubora unaoendana na thamani ya fedha zilizoletwa, lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wake, wanapata huduma bora kupitia miradi hiyo, kama ilivyokusudiwa na Serikali ya awamu ya tano.

Aidha Mkurugenzi huyo, amewataka wananchi wa maeneo wanayonufaika na miradi hiyo, kujitoa kuchangia nguvu kazi ya asilimia 10, kama miongozo ya miradi ya TASAF inavyoelekeza, ili utekelezaji wa miradi hiyo uende kwa kasi na kukamilika kwa wakati, zaidi waweze kupata miradi mingine zaidi.

"Katika miradi hii, wananchi wanapaswa kujitolea nguvu kazi kwa asilimia 10, hivyo niwaombe  wananchi wangu wa Laroi, Lemuguru na Losikito, kujitolea nguvu kazi hiyo, ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati, na Serikali iweze kutuletea miradi mingine zaidi, kwa faida yetu wenyewe" amesisitiza Mkurugenzi huyo.

Akizungumza kwa niaba ya Mratibu wa TASAF halmashauri ya Arusha, Kabula Sukwa, amefafanua kuwa, tayari mchakato wa kupata wakandarasi wa kutekeleza miradi hiyo uko hatua za awali, na mara baada ya kukamilika hatua zote, miradi itaanza kutekelezwa, na kuongeza kuwa miradi yote hiyo, inategemewa kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha wa 2019/2020.

Hata hiyo, Kabula amezitaja gharama za kila mradi ni pamoja na ujenzi wa nyumba mbili za walimu zenye sehemu mbili (2 in 1) zitakazogharimu kiasi shilingi milioni 144.58 huku kila nyumba ikigharimu shilingi milioni 72.29 na mradi wa ujenzi wa kivuko cha Laroi ukigharimu kiasi cha shilingi milioni 72.38 na kufanya gharama za miradi yote mitatu kuwa ni shilingi milioni 216.98

Jumla ya vijiji 45 vya halmashauri ya Arusha, vinanufaika na miradi ya TASAF awamu ya tatu, kupitia miradi yake ya OPEC, huku takribani kaya  9045 zikinufaika mradi wa Uhawilishaji fedha kwa kaya  masikini.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.