• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wajapani watua na teknolojia ya kuondoa madini ya Floraidi kwenye maji kwa kutumia nyuzi za pamba.

Posted on: March 3rd, 2019

Watalamu wabobezi wa tafiti na teknolijia ya kutibu maji, wametua katika halmashauri ya Arusha, kwa lengo la kuhawilisha teknolojia ya kutibu maji na kuondoa kiwango cha madini ya Floraidi kwa kutumia nyuzi za pamba, wakitokea chuo kikuu cha Shinshu cha nchini  Japani.

Wabobezi hao kutokea nchini Japani, wamepata fursa ya kukutana na kufanya mhadhara na wadau wa sekta ya maji, ndani na nje ya halmashauri hiyo, wenye lengo la kuwa na uelewa wa pamoja wa teknolojia mbalimbali za kutibu maji, mhadhara uliofanyika kwenye hoteli ya Mount Meru jijini Arusha, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mdahalo huo, Katibu Tawala mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, ameelezea hali halisi ya upatikanaji wa maji katika mkoa wa Arusha, na kuthibitisha uwepo wa changamoto kubwa ya madini ya Floride kwenye maji ya ukanda huo.

Amesema kuwa, licha ya kuwa serikali imefanikiwa kusambaza maji vijijini kwa asilimia 63 mpaka sasa, lakini bado baadhi ya maeneo, kuna tatizo la uwepo wa kiwango kikubwa cha madini ya Floraidi kwenye maji kulinganisha na kiwango kinachofaa kwa binadamu kilichotolewa na Umoja wa Mataifa, madini ambayo yana madhara kwa bianadamu.

Kwitega afafanua kuwa, takwimu zinaonesha takribani asilimia 42 ya vyanzo vya maji katika mikoa ya Arusha, Shinyanga, Singida na Manyara, vimeathiriwa na uwepo wa madini ya Floraidi iliyozidi kiwango cha kimataifa kinachokubalika na Shirika la Afya Duniani cha miligramu 1.5 kwa lita.

Kutokana na takwimu hizo, Kwitega amesema, ni dhahiri kuwa miradi mingi ya ya maji iliyopo na inayoendelea kujengwa mijini na vijijini katika mikoa hiyo, inahitaji mifumo na miundo mbinu bora na rahisi ya kutibu maji na kuondoa kiwa cha madini hayo y a Floraidi kwa ajili ya usalama wa afya za wananchi.

Hata hivyo wajapani hao, wameelezea aina tofauti za teknolojia ya kutibu maji na kuondoa madini yote yasiyo rafiki kwenye maji, ikiwemo madini hatari ya Floraidi, teknolojia inatumia baadhi ya malighafi zinazopatikana hapa nchini.

Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Sayansi na Teknolojia nchini Japani, Profesa  Yoshiko Shirokizawa, Mlamu mbobezi wa masuala ya utafiti kutoka  chuo kikuu cha Shunshi cha nchini Japa, amesema kuwa, teknolojia hiyo ya kuondoa madini ya floraidi, inatumia nyuzi za pamba, malighafi ambayo inapatikata kwa wingi hapa Tanzania.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera, amethibitisha uhutaji mkubwa waa teknolojia ya kuondoa madini ya floraidi kwenye maji katika halmashauri yake, kutokana na uwepo wa watu walioathirika na madini hayo katika kijiji cha Lemanda kata ya Oldonyosambu.

Aidha mkurugenzi Mahera amefafanua kuwa, teknolojia iliyoelekezwa na wajapani hao inaonekana ni nzuri japo kuwa bado ina uwezo wa kutibu maji kwa kiwango kidogo, wakati hitaji la  halmashauri kwa sasa ni teknolojia rahisi ya kuondoa madini hayo, kwa kutibibu kiasi kikubwa cha maji kwa wakati mmoja na kushauri kuwa, watalamu hao kutoka Japani kushirikiana na kituo cha kufanyia tafiti cha Tanzania na kufanya tafiti zaidi kwa pamoja ili kuweza kupata njia nzuri zaidi ya kuondoa madini ya floraidi iliyozidi kwenye maji kwa kutibu kiasi kikubwa cha maji.

Aidha amewataka wajapani hao kuwahusisha na kuendelea kutoa mafunzo zaidi kwa wadau na watalamu wa maji wa kitanzani juu ya uendeshaji wa teknolojia hiyo na kuwafanya kuifahamu zaidi teknolojia hiyo.


PICHA ZA MATUKIO KIKAO KAZI









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.