• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAJUMBE WAWAJUMBE WA MABARAZA YA USULUHISHI YA KATA YATAKIWA KUFANYAKAZI KWA KUZINGATAI TARATIBU ZILIZOAINISHWA.....

Posted on: June 26th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wajumbe wa Mabaraza ya Usuluhishi ya kata, wametakiwa kufanyakazi kwa kuzingatia taratibu zilizoainishwa kwenye miongozo iliyotolewa na serikali, ili kufanya mashauri kwa weledi na kwa kuzingatia haki.


Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, wakati wa mafunzo ya siku mbili ya wajumbe hao, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano shule ya msingi Green Acres kwa kuwataka wajumbe hao, kutambua kuwa wanaufungua ukurasa mpya wa kwa kufanya usuluhishi wa migogoro ya ardhi kwenye maeneo yao.

Mkurugenzi Msumi amewataka wajumbe hao kutumia busara na hekima katika kufanya usuluhishi kwa  kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za Mabaraza ya usuluhishi, na pale inapotokea sintofahamu rudini kwenye miongozo inayowaelekeza nini cha kufanya.

"Mafunzo mliyopewa yazingatieni ili tukatende haki kulingana na taratibu zilizowekwa, majukumu mliyokasimiwa yanagusa maslahi ya jamii, familia na mtu mmoja mmoja kwa kutambua kanda hii ya Kaskazini hususan mkoa wa Arusha  kuna migogoro mingi ya ardhi, kutokana na ufinyu wa ardhi usioendana na idadi ya watu, ni vymea kuzingatia taratibu za usuluhishi" AmesemaMsumiA

Aidha amewataka wajumbe hao, kutambua kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha migogoro ya ardhi inatatuliwa kuanzia ngazi ya kijiji, kata na wilaya, hivyo  jukumu kubwa wanalotakiwa kulitekeleza ni kwa manufaa ya  wananchi na nchi kwa ujumla.Kwa sasa mambaraza yanafanya kazi ya usuluhishi na upatanishi na sio maamuzi, maamuzi yanatakiwa kuoelekwa kwenye ngazi nyingine za maamuzi kulingana na sheria na miongozo .             

Hata hivyo wajumbe hao wameishukuru na kuipongeza serikali kwa mafunzo hayo na kuweka wazi kuwa miongozo na taratibu walizopewa zimewapata maarifa mapya, ambayo yatakuwa nguzo yao katika utendaji wa kazi zao za usuluhishi wa migogoro ya ardSes

Sesilia Msingwa mjumbe wa Baraza la Usuluhishi kata ya Oldonyosambu amesema kuwa mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa kutambua namna ya kufanya usuluhishi kwa kuzingatia haki ya kila upande bila upendeleo na kuwafanya kujiamini na kutenda haki kwa watu wakati wa kufanya usuluhisMa.

"Mafunzo haya yametupa mwanga wa namna bora ya kusuluhisha migogoro kwa kuzingatia kanuni na taratibu, na zaidi yametuelekeza mipaka ya wajumbe kwamba kazi yao ni usuluhishi na si kufanya maamuzi" Thomas Kisioki Katibu Baraza la Usuluhishi kata ya Laroi


Hata hivyo Mkuu wa Kitengo cha Sheria, halmashauri ya Arusha Monica Mwailolo amesema kuwa, mafunzo hayo ni muhimu, yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo wajumbe wa Mabaraza ya usuluhishi ya kata, Mabaraza ambayo yamepewa jukumu la usuluhishi wa migogoro ya Ardhi kulingana na Sheria ya Mabaraza ya Kata sura ya 206 na Sheria ya Mahakama za Ardhi sura ya 216.  

Aidha amewataka wajumbe hao, kufanyakazi kwa karibu na kitengo cha sheria ili kuweza kutatua changamoto zozote zitakazojitokeza wakati wa mashauri. 

"Niwatake wajumbe kuzigatia taratibu zilizowekwa kwa kuwa ndio nguzo zitakazowawezesha kufikia malengo ya kusuluhisha migogoro ya ardhi katika maeneo yenu" Amefafanua Mwanasheria Monicai

Awali uongozi wa halmashauri unawashukur wadau wote walioshiriki kuandaa mafunzo hayo, wakiwemo shirika la SOS Children, CWCD, PRINGO'S, Kituo cha Haki za Binadamu .


ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.