• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WALENGWA WA TASAF WANAOJIMUDU KUONDOLEWA KWENYE MPANGO WA KAYA MASIKINI

Posted on: August 28th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Mtalamu ufuatiliaji kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF makao makuu, Judith Masika, amewasilisha utaratibu na maelekezo ya Serikali kupitia TASAF, wa kuanza mchakato maalumu kuwaondoa kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini, walengwa walioboreka kutokana na mpango huo na kukidhi vigezo vya kuweza kujitegemea, pamoja na kuanza malipo  kupitia mfumo wa kielektroniki na kuondoa malipo ya fedha taslimu.

Mratibu huyo, amewalezea Waheshimiwa Madiwani wakati wa mkutano wa Baraza la Kata, uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha kuwa, kutakuwa na  zoezi maalum la kuwaondoa walengwa ambao wamekidhi vigezo kwa kuwa tayari wamekuwa na uwezo wa kuanzisha miradi inayowawezesha kujikimu kimaisha ili nafasi hizo zichukuliwe na walengwa wenye sifa ambao hawako kwenye mpango na wanakidhi vigezo vya kuingizwa kwenye mpango huo wa kunusuru kaya masikini.

"Zoezi hili litahusisha walengwa wa TASAF ambao tayari wameweza kujikimu kimaisha kwa kuanzisha miradi ambayo inawawezesha kupata mahitaji yao muhimu ya kimaisha na kukidhi vigezo vya kutokuwa kaya masikini tena, pamoja na baadhi ya walengwa kuingizwa kwenye mpango wakiwa hawana sifa, kwa kuwa wanauwezo na tunawafahamu kwa kuwa tunaishi nao katika maeneo yetu" Amesisitiza Judith

Aidha amelezea mabadiliko ya utaratibu wa serikali kupitia TASAF, wa kuwasajili walengwa kwenye mfumo ili waweze kulipwa ruzuku ya fedha kwa njia ya kielektroniki kupitia mitandao ya simu, benki na mawakala wa mitandao ya simu na kuachana na utaratibu uliopo wa kulipa fedha taslimu.

Amefafanua kuwa utaratibu wa kuwaondoa walengwa hao, utafanyika kupitia mkutano mkuu mkuu wa kijiji, na utahusisha walengwa wote walio kwenye mpango, kwa kuwasajili kwenye mfumo kupitia vitambulisho vyao vya Taifa (NIDA) na kusajili  namba zao za simu na kwa walengwa wasio na simu wala akaunti za benki watatumia mawakala wa simu waliopo kwenye maeneo yao

Hata hivyo waheshimiwa madiwani walibainisha changamoto za maeneo yasiyo na mtandao ya simu, wazee wasio na simu na wale wasiojua kusoma na kuandika, wagonjwa na kaya ambazo zinaongozwa na watoto wasio na wazazi.

Mratibu huyo amefafanua kuwa, kwa walengwa ambao ni wazee sana, wasiojua kusoma na kuandika, wagonjwa, na kaya zinazoongozwa na watoto zitahudumiwa kupitia mawakala ambao wanasimamiwa na uongozi wa TASAF pamoja na program ya wasimamizi wa walengwa watakaochaguliwa kutoka kwenye jamii husika.

Aidha ameweka wazi faida za malipo kwa njia ya  kielekroniki ni pamoja na usalama wa fedha za walengwa na kuondoa wizi na upotevu wa fedha, hali za udanganyifu, pamoja na kuwapa fursa walengwa kufanya maamuzi sahihi ya matumizi ya fedha, huku ikiokoa muda kwa walengwa badala ya kupanga foleni kusubiri fedha,watatumia muda huo kufanya shughuli nyingine za maendeleo za kuwaingizia kipato.

Awali, amewataka madiwani hao, kushirikiana na wananchi, uongozi wa vijiji katika maeneo yao, na kuwa mabalozi wazuri kwa kuweleimisha wananchi kutambua umuhimu wa zoezi hilo, lenye manufaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.


ARUSHA DC 

KAZI INAENDELEA


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.