• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WADAU WATOA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE KWA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI MATIMU

Posted on: January 25th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wanafunzi 1,544 shule ya msingi Matimu halmashauri ya Arusha wamepata msaada wa vifaa vya shule kutoka kwa Kampuni ya Utalii la Masaai Wounders la Jijini Arusha.


Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo, Mkurugenzi Mkazi, Mwl. Ang'weni Lang'o,  amebainisha kuwa, lengo la kugawa vifaa hivyo ni baada ya kuona changamoto inayowakabili baadhi ya wazazi ya kushindwa kumudu kuwapatia watoto wao vifaa vya shule.


Amesema kuwa kutokana na changamoto hiyo shirika likaona ni vema kuwapunguzia wazazi mzigo huo ili watoto waweze kupata nafasi ya kuhudhuria masomo yao bila kikwazo.


"Leo tumetoa sare za shule kwa wanafunzi wote 1,544 wa shule hii,  jozi 1300 za viatu, mashati, sketi, suruali na masweta, nguo za michezo na vifaa vya michezo, pamoja na vitabu vya kiada kwa shule jirani ya sekondari  Mukulat" . Amesema Mwl. Lang'o.


Naye mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi na Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Elizabeth Ngobei licha ya kulishukuru shirika hilo amewataka wanafunzi kutumia fursa hiyo adhimu kusoma kwa bidii kwa kuwa, tayari wadau kwa kushirikiana na Serikali, wameshafanya sehemu kubwa ya majukumu yao.


Amewataka kutambua kuwa wapo watoto wenzao wanaoshindwa kuhudhuria shule kwa kukosa vifaa vya shule, na kuwasisitiza kuthamini fursa hiyo waliyopata kwa kuongeza bidii katika masomo yao ili kuzifikia ndoto zao.


"Wazazi mnalojukumu kubwa kuwasimamia watoto hawa kutunza vifaa hivi lakini walimu mnao wajibu wa kuhakikisha mnawafunfisha wanafunzi hawa ili waweze kufaulu vema na kufikia" Amesisitiza Elizabeth.


Hata hivyo wanafunzi hao wameshukuru shirika kwa misaada mingi inayotolewa shuleni hapo na kuahidi kusoma kwa bidii kwa kuwa shule yao ina mazingira mazuri na rafiki ya kujifunzia tofauti na shile nyingine za msingi.


Upendo Paulo mwanafunzi wa darasa la VI, amesema ndoto yake ni kuwa daktari hivyo ameahidi kusoma kwa bidii na kufikia ndoto yake kama ilivyo kwa watoto wengine wanaosoma shule za kulipia.


"Shule yetu ni nzuri sana, haina tofauti na shule za 'English Medium', mazingira ni mazuri, tuna vitabu, vifaa vya michezo na leo tumepewa uniform, kazi yetu ni kusoma kwa bidii". Ameweka wazi Enock Eliasi darasa la VI.


Hata hivyo Mwenyekiti wa Kamati ya shule Philemon Loth, hakusita kuwashukuru wadau hao kwa mambo makubwa wanayoyafanya shuleni hapo, na kuahidi kushirikiana na walimu kuhakikisha watoto wanahudhuria shule pamoja na kufanya vizuri katika masomo.


"Tunawashukuru wadau wetu, zaifi pia tunaishukuru Serikali yetu kwa kuweka mazingira rafiki kwa wadau na kufikiwa na msaada huu, sisi kama wazazi tunauthamini na tunaahidi kuwahimiza watoto wetu kuongeza bidii kwenye masomo kwa manufaa yao na Taifa". Amefafanua Mwenyekiti huyo.


Kampuni ya Masaai Woundering imekuwa ikitoa misaa mingi katika shule hiyo, ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya shule, chakula cha walimu na wanafunzi, vifaa na vitabu vya kufundishia na kujifunzia, pamoja na vifaa vya michezo.


ARUSHA DC Yetu, Tushirikiane Kuijenga'

KaziInaendelea ✍✍










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.