• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI ARUSHA DC WASISITIZWA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA ILIYOBORESHWA

Posted on: February 3rd, 2021

Na.Elinipa Lupembe.

Wananchi halmashauri ya Arusha wametakiwa kuunga mkono juhudi za serikali yao, kwa kutumia vituo vya afya vinavyojengwa katika maeneo yao kwa kujiunga kwenye mfuko wa  Bima ya Afya - CHF iliyoboreshwa, ili kurahisihsa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo hivyo vya kutolea huduma za afya.

Rai hiyo imetolewa na wajumbe wa Kamati ya Siasa wilaya ya Arumeru wakati walipofanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika halmashauri ya Arusha, ikiwa na lengo la kukagua utelelezaji wa Ilani ya Chama cah Mapinduzi kwa vitendo, kuelekea maadhimisho ya miaka 44 tangu kuzaliwa kwa CCM Februari, 1977.

Wajumbe hao wamesema kuwa serikali ya awamu ya tano imejikita katika kutatua kero za wananchi hususani katika sekta ya afya, kwa kujenga zahanati na vituo vya afya, lengo likiwa ni  kuwasogezea wananchi huduma za afya katika maeneo yao, sambamba na kurahisisha upatikanaji wa matibabu, pamoja na kupunguza vifo vya mama hasa kwa wananchi waishio vijijini.

Wakizungumza na wananchi wa kata ya Musa, wakati wakikagua maendeleo ya  mradi wa Zahanati ya Musa uliyojengwa kwa fedha za EP4R, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha, Steven Zelote, amewataka wanachi kuhakikisha kila kaya, inakuwa na kadi ya BIMA ya Afya - CHF iliyoboreshwa, ili kufikia malengo ya serikali ya kuwapatia wananchi huduma muhimu za afya katika maeneo yao, kwa kuwa tayari serikali, imejenga zahanati na vituo vya afya katika mmaeneo yao. 

Mwenyekti Zelote amefafanua kuwa, serikali imetekeleza jukumu lake la kujenga zahanati na vituo vya afya katika maeneo ya vijijini, ni  wajibu wa wananchi sasa kutumia zahanati hizo, kwa kutekeleza mpango wa kukata kadi za kadi za Bima ya Afya na kuwa na uhakika wa kjtibia pindi wanapougua,  ili kwenda sambamba na lengo la serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na chama makini cha CCM, lengo la kuwahudumia wananchi wanyonge kwa gharama nafuu.

"Kwa miaka 44 ya CCM kuongoza serikali ya Tanzania, wananchi wamekuwa na imani na chama hicho, kutokana na mafanikio makubwa ya kimaendeleo hususani katika kufikisha huduma za afya vijijini, hii inaweka wazi kuwa CCM ni chama imara, chenye uongozi imara kinachoongoza serikali imara yenye kuwajali wananchi wote" amesisitiza Mwenyekiti Zelote.

Naye Emmanuel Memutiye, mkazi wa kijiji cha Oloitushula, amelalamikia uwepo wa changamoto za matumizi ya Kadi za Bima za Afya, pindi inapomaliza muda wake, na kusababisha wagonjwa kukosa matibau kutokana na kadi hizo kumalizika muda wake.

Hata hivyo, kwa kujibu changamoto hizo, Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Arusha, Saad Mtambule, amewataka wananchi kuhakikisha wanafahamu muda wa mwisho wa matumizi ya kadi zao, na kuandaa mapema utaratibu wa kuzihuisha kadi hizo kabla ya kumalizika kwa muda wa matumizi ya kadi hizo.

"Ni vema kila mwenye kadi ya BIMA kufahamu muda wa kumalizika kwa kadi yake, na kujiandaa kuzihuisha 'kurenew' kabla ya muda wa mwisho wa matumizi yake, ili kuepusha changamoto za kushindwa kupata matibabu pindi mwanakaya anapougua, kwa kuwa kadi hizo zimeingizwa kwenye mfumo ambao ikiisha muda wake haiwezi kutumika, mfumo unaikataa" amesema Mkurugenzi Mtambule.

Awali wananchi wa kata ya Musa wamethibitisha, mafanikio makubwa ya ujenzi wa zahanati hiyo ya Musa, kwamba uwepo wa zahanati hiyo, umeleta mafanikio makubwa kwa wananchi wa Musa hasa wanawake na watoto, kutokana na ukweli kwamba kumeokoa na kupunguza vifo vya wanawake na watoto wakati wa kujifungua pamoja na kuongeza kasi ya wajawazito na watoto kuhudhuria kliniki kwa wakati.

Asnath Simoni mhudumu wa afya ngazi ya Jamii, amethibitisha kuwa, kumekuwa na mwamko mkubwa wa wajawazito kuhudhuria  kliniki pamoja na kujifungulia kwanye zahanati, tofauti na hapo awali, wajawazito walikuwa hawahudhurii kliniki na kujifungulia nyumbani, jambo ambalo lilihatarisha afya na maisha ya wajawazito na watoto.

Ziara hiyo ya Kamati ya Siasa wilaya ya Arumeru, imefanikiwa kukagua jumla ya miradi 5 katika sekta ya afya, elimu, maji na miundombinu ya barabara,  ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020/2025, ikiwa ni muendelezo wa shughuli za Chama za kuelekea maadhimisho ya sikukuu za miaka 44 tangu kuzaliwa chama hicho, zitakazofanyika tarehe 06.02.2021.


PIICHA ZA MATUKIO YA UKAGUZI WA MIRADI ILIYOTEMBELEWA NA KAMATI YA SIASA WILAYA YA ARUMERU.
















Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.