• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wananchi waungana na serikali kujenga choo kilichototia shule ya Msingi Seliani

Posted on: October 26th, 2018

Kufuatia tukio la ajali ya kutitia kwa choo katika shule ya msingi seliani, kata ya Kimnyaki, Halmashauri ya Arusha wilayani Arumeru mkuu wa wilaya hiyo Mheshimiwa Jerry Muro, ameendesha harambee ili kupata fedha za ujenzi wa choo kipya na cha kisasa.

Katika zoezi hilo Mh.Muro amechangia kiasi cha shilingi laki tano na kuungwa mkono na wananchi wa eneo hilo kuchangia fedha na kufanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi milioni moja na kuwezesha ujenzi wa choo hicho kuanza mara moja siku ya Jumatatu ijayo na wanafunzi waweze kupata huduma hiyo.

Mkuu huyo wa wilaya amemuagiza mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha, kuanza mchakato wa dharura wa kupata vifaa vya ujenzi ikiwemo matofali na saruji kwa ajili ya kuanza ujenzi wa choo hicho na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya Jumatatu kwa ajili ya kujitolea kushiriki shughuli za ujenzi huo kwa hali na mali.

“Tukio hili ni la kwetu sote niwaombe wananchi kuwa watulivu, serikali yenu itashirikiana nanyi kuhakikisha choo kinajengwa na watoto wetu wataendelea na masomo yao kama kawaida”. Alisema Muro.

Wakati huo huo, Mh. Muro ameuomba uongozi wa kanisa la KKKT, Usharika wa Seliani kuwaruhusu wanafunzi kutumia choo cha kanisa hilo, kwa kipindi cha wiki moja ambacho serikali na wananchi wanapolishughulikia ujenzi wa choo hicho.

Akitoa taarifa ya ajali hiyo, mwakilishi wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji,  Sajenti Isaac Mollel, amesema kuwa, wamefanikiwa kumuokoa mwanafunzi mmoja wa darasa la kwanza Emanuel Zakaria (7) aliyekuwa chooni wakati wa tukio hilo, na kukimbizwa hospitali ya Seliani Ngaramtoni kwaajili ya matibabu. 

Hata hivyo kwa mujibu wa Dkt. Mfawidhi hospitali ya Selian, mtoto huyo hakupata athari kubwa na anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Samweli Mollel ameelezea chanzo cha ajalo hiyo,  ni kutokana na miundo mbinu ya  choo hicho, kuwa ya ya zamani iliyojengwa miaka mingi iliyopita, licha ya choo hicho kuwa na matundu machache kwa kulinganisha na idadi ya wanafunzi.

Mollel amethibitisha ushiriki wa wananchi wa kijiji hicho kwa serikali, katika ujenzi wa choo cha kisasa, chenye kujengwa shimo nje ili kuepuka madhara mengine kama hayo kutokea tena.

“Choo kilijengwa kizamani lakini kwa sasa tutahakikisha tunajenga choo bora cha kisasa, ambacho shimo lake litakuwa nje tofauti na la awali ili watoto wetu wasisumbuke tena” Amesisitiza Mwenyekiti huyo.

Tukio la kutitia kwa choo cha wanafunzi wa shule ya msingi Seliani, lilitokea majira ya saa tatu na nusu asubuhi, huku chanzo kikuu kikielezwa kuwa ni miundombinu chakavu ya choo hicho baada ya kutumika kwa muda mrefu na tayari wananchi wameshaanza kuchanga fedha kwaajili ya ujenzi wa choo kipya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.