• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAUME MSINGI WA MABADILIKO YA MILA POTOFU ZINAZOSABABISHA UKATILI DHIDI YA WATOTO WA KIKE

Posted on: July 2nd, 2021

Elinipa Lupembe.

Wanaume katika jamii, wamehimizwa kusimama imara kutokomeza na kuachana na mila potofu zinazosababisha vitendo vya ukatili dhidi ya watoto, hususani watoto wa kike,  dhamana ambayo iko mikononi mwa wanaume ambao ni viongozi wa familia na viongozi wa mila pia.

Hayo yamesemwa na Kaimu mkurugenzi, halmashauri ya Arusha, mwalimu Hossein Mghewa, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya kupinga ukatili dhidi ya watoto, ukatili unaosababishwa na mila na desturi potofu za jamii, mafunzo yaliyoandaliwa na Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na watoto, Idara ya Ustawi wa Jamii, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.

Kaimu mkurugenzi huyo, amesema kwamba, wanaume ndio viongozi na nguzo kuu za familia, na viongozi wa mila, hivyo wakiamua kubeba dhamana ya kufanya mabadiliko ya kijamii ya kuachana na mila potofu zinazosababisha ukatili dhidi ya watoto, vitendo hivyo vitapungua kwa kasi na hatimaye kutokomea kabisa.

Ameweka wazi kuwa, wanaume ndio watawala na wafanya maamuzi kuanzia ngazi ya familia na jamii, endapo  wakiamua kwa pamoja kubadilika na kuachanan na mila hizo potofu za kukeketa na  kuwaozesha watoto wa kike  katika umri mdogo, ukatili  utatoweka kabisa na kubaki historia kwenye jamii za kimaasai.

"Kama kila mwanaume ndani ya familia akisema, mtoto wangu wa kike, hatakeketwa wala kuolewa katika umri mdogo, hakuna anayeweza kupinga, na zaidi wale viongozi wa mila wakiamua ni marufuku mtoto wa kike kukeketwa, na wanaume wote wakatae kuoa msichana aliyekeketwa, mila hiyo itatokomea na wanawake watatii na jamii nzima itafuata na hatimaye ukatili huo utakwisha ndani ya jamii zetu". Ameweka wazi Kaimu huyo Mkurugenzi

Aidha ametoa wito kwa washiriki wote wa mafunzo hayo, kuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya ukatili katika maeneo yao, pamoja na kutumia maarifa waliyoyapata kushirikiana na serikali kuelimisha jamiii juu ya madhara ya ukatili dhidi ya watoto na kutoa taarifa katika mamalaka husika pindi mtoto atakapofanyiwa ukatili.

Hata hivyo washiriki wa mafunzo hayo licha ya kuipongeza serikali kwa kuandaa mafunzo hayo yaliyowapa maarifa kwa uwanda mpana, maarifa yaliyowawezesha kufahamu madhara ya ukatili kwa watoto na namna ya kupambana na ukatili, kwa kujikita kuelimisha jamii kila mtu kwa nafasi yake aliyonayo katika jamiii, lakini pia wamekiri kuwa wanaume wanayo dhamana kubwa ya kuweza kuleta mapinduzi ya kuachana na mila potofu za ukeketaji na ndoa za utotoni.

Mwenyekiti wa mafunzo hayo, Mchungaji Ezekiel Megiroo wa kanisa la KKT usharika wa Kisongo, Mchungaji Ezekiel Megiroo kutoka kkt Kisongo,  amekiri kuwepo kwa vitendo vya ukatili vinavyofanywa na watu wa ndani ya familia na kuongeza kuwa,  jamii inahitaji kupata elimu zaidi juu ya madhara makubwa ya ukatili huo, na  kupitia mafunzo hayo na kutekeleza  mpangokazi  uliowekwa kwa weledi, utapunguza matukio ya ukatikli kwa asilimia kubwa

"Tuko tayari kutumia majukwaa yetu,  kueleimisha jamii hususani  wanaume ambao ndio viongozi wa familia, kubadili mitazamo  yao na kuachana na mila potofu, jambo ambalo ninaamini litasaidia kuondokana na ukatili dhidi ya watoto kuanzia ngazi ya familia na jamii kwa ujumla wake"amesisitiza mchungaji Megiroo.

Naye mratibu wa mafunzo hayo, kutoka Wizarla ya Afya na Maendeleo ya Jamii, Imeldaevaeline Kamugisha, amesema kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kujengeana uelewa wa pamoja wa kutokomeza ukatili dhidi ya watoto, na kuandaa  mpango kazi kwa mwaka, ambao utafanyiwa fuatilaji wa utekelezaji wake mara kwa  malrai ili kupata matokeo chanya na kufikia lengo la serikali la kuotokomeza ukatili unaokabili watoto katika jamii.

Mafunzo hayo ya siku tatu, yamejuisha watalamu wa Ustawi na Maendeleo ya Jamii na halmashauri ya Arusha, wajumbe wa kamati ya MTAKUWAA, polisi wa Dawati la Jinsia, Afisa Uhamiaji, walimu wa mangariba, wawakilishi wa makundi ya kijavmii, wadau wa mashirika yanaoyojihusisha na masuala ya ukatili, viongozi wa  dini pamoja na viongozi wa mila. 

ARUSHA DC

Kazi inaendelea✍✍


Kaimu mkurugenzi halmashauri ya Arusha, mwalimu Hossein Mghewa akifunga mafunzo ya siku tatu ya  kupambana na ukatili dhidi ya watoto, mafunzo yaliyoandaliwa na Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri ya Arusha.

Mwenyekiti wa washiriki wa mafunzo mchungaji Ezekiel Megiroo wa kanisa la KKT usharika wa Kisongo, akizungumza wakati wa kuahirisha mafunzo hayo ya siku tatu.

Mratibu wa mafunzo kutoka Wizara ya Afya -Idara ya Ustawi wa Jamii, Imeldaevaline Kamugisha akizungumza wakati wa kufunga mafunzo.








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.