• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANUFAIKA WA MIKOPO ISIYO NA RIBA WATAKIWA KUFANYA MIRADI YENYE TIJA ILI KUWEZA KUFANYA MAREJESHO

Posted on: December 23rd, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wanufaika wa mikopo isiyo na riba ya asilimia 10 ya mapato ya ndani inayotolewa na halmashauri kwa vikundi vya vijana, kina mama na walemavu, wametakiwa kufanya shughuli za uzalishaji zenye tija na zitakazoleta faida ili kupata faida na kumudu kurejesha mikopo hiyo.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Arusha, Angela Mvaa wakati walipokutana na wanavikundi hao kwaajili ya kusaini, mikataba ya kupokea fedha hizo, fedha ambazo zitarejesha kwa kipindi cha mwaka mmoja, katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Afisa Maendeleo huyo amebainisha kuwa ni vema kila kikundi kujikita kwenye shughuli za mradi ambao mmewasilisha kwenye andiko na kusimamia mradi huo ili uweze kuleta faida kwa manufaa ya familia na kurejesha deni pia.

Aidha amesema kuwa, ni muhimu kila mwanakikundi kutambua masharti ya mkopo unaotolewa na Serikali ya Awamu ya sita na kuwajibika ipasavyo kufanya shughuli za miradi iliyokusudiwa ili fedha hizo ziweze kurudishwa kwa wakati na kusisitiza utunzaji wa kumbukumbu za matumizi yote ya fedha ili kuepuka upotevu wa fedha za Serikali.

“Mikopo hii inatolewa kwa watu waliokidhi vigezo kulingana na kiasi cha fedha kilichopo na si vinginevyo, ninyi mna sifa na mmekidhi vigezo vya kupata mkopo huu, niwaombe kuepuka matumizi yoyote yasiyo ya lazima ili muweze kufikia malengo yenu na kurejesha fedha hizo kwa wakati.” Alisisitiza Mvaa.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii dawati la vijana halmashauri ya Arusha, Ahadi Mlay amesema kuwa lengo la Serikali kutoa mikopo hiyo isiyo na ribariba, walemavu, vikundi vya vijana na akinamama ni kutoa fursa kwa jamii kuinuka kiuchumi kupitia shughuli mbalimbli za uzalishaji ikiwa ni pamoja na kuzakuza ajira hasa kwa vijana ambao wanapitia changamoto ya kukosa mitaji ya kuanzisha biashara.

“Fedha hizi sio kwa ajili ya kugawana kwa kila mwanakikundi na kila mtu kufanya mradi anaotaka bali ni kwaajili ya kufanya mradi uliokusudiwa na wanakikundi wote kwa pamoja na faida itakayopatikana ndiyo inapaswa kugawanywa kwa kila mwanakundi.” Ameweka wazi Mlay.

Hata hivyo wanufaika hao wameishukuru Serikali ya Awamu ya sita, inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali, wananchi wake na kuwapatia fursa nyingi za kujikwamua kiuchumi pamoja na kuzalisha ajira kwa watanzania waliokuwa wamekata tamaa ya kujiendeleza, kiuchumi kutokana na kukosa mitaji ya kufanyia biashara.

“Matamanio yangu ni kukuza biashara yangu ya nafaka, matunda na mbogamboga na kuwekeza zaidi ili niweze kuwa mfanyabiashara mkubwa, ninaishukuru sana Serikali kwa kutupatia fursa hii addhimu na ninawashauri na watanzania wengine kuchangamkia fursa hii masharti yake siyo magumu na hakuna ubaguzi.” Alisema Michael Thomas ambaye ni mlemavu wa Kata ya Mateves, mara baada ya kusaini mkataba wa mkopo

Awali, halmashauri ya Arusha imetoa shilingi milioni 217 kwa vikundi 15 ambapo, fedha hizo zinatarajiwa kurejeshwa kwa kipindi cha ndani ya miaka mitatu.


ARUSHA DC

KaaiInaendelea ✍













Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.