Na. Elinipa Lupembe.
Jumla ya watahiniwa 5,832 halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru, wanategemea kuanza mitihani yao ya Taifa kesho Jumatatu, mitihani ya kuhitimu kidato cha nne mwaka 2019.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Alvera Ndabagoye, amesema kuwa, watahiniwa hao, watafanya mitihani hiyo kwenye shule za sekondari 48, ndani ya halmashauri hiyo na kuwataka watahiniwa na wasimamizi wote, kuepuka aina yoyote ya vitendo vya udanganyifu badala yake kufuata kanuni, taratibu, Sheria na miongozo yote ya mitihani ya Taifa ikiwa ni pamoja na kuzingatia taratibu za watahiniwa wenye mahitaji maalum.
Aidha amethibitisha kuwa, maandalizi yamekamilika, na wanategemea kuanza mitihani hiyo kesho, kufuatia ratiba iliyotolewa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) na kuthibitisha kuwa watahiniwa wote wameandaliwa vizuri kisaikolojia na wanategemea kufanya mitihani yao kwa amani na utulivu.
Hata hivyo, Afisa Elimu Sekondari, halmashauri ya Arusha, mwalimu Menard Lupenza, amefafanua kuwa, watahiniwa watakaofanya mitihani hiyo ni pamoja na watahiniwa wa shule (school canditates), watahiniwa wakujitegemea (private candidates) pamoja na watahiniwa wa Maarifa (QT).
Aidha ametaja idadi ya watahiniwa wa shule ni 5,058, ikiwa wavulana 2,115 na wasichana 2,943, watahiniwa wa kujitegemea ni 680 huku watahiniwa wa Maarifa - (QT) ni 94 na kufanya, halmashauri ya Arusha, kuwa na jumla ya watahiniwa 5,832 kwa mwaka 2019.
Aidha Afisa Elimu Lupenza, amethibitisha kukamilika kwa maandalizi na halmashauri kuwa na mategemeo ya watahiniwa hao kuleta matokeo mazuri, kutokana na mkakati wa kutokomeza alama sifuri kwa watahiniwa wote.
Aidha, Halmashauri ya Arusha inawatakia watahiniwa wote, kila la Kheri katika mitihani yao, kufanya mitihani kwa amani na utulivu ili kupata matokeo mazuri.
RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2019
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.