• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wazabuni wa uzoaji taka Arusha DC, watakiwa kutoa huduma bora na stahiki kwa jamii

Posted on: January 22nd, 2019

Na.Elinipa Lupembe

Wazabuni wa kukusanya takataka katika maeneo mbalimbali ya halmashauri ya Arusha,wilayani Arumeru, wametakiwa kutambua kuwa kazi wanayoifanya ni ya kutoa huduma bora na stahiki kwa jamii na si kujikita na kuweka mbele  zaidi maslahi wanayoyapata.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera, alipokutana na wazabuni hao ofisini kwake, mapema wiki hii kwa lengo la kujadili njia bora ya utoaji huduma pamoja na changamoto zinazoikabili sekta hiyo, hususani katika swala zima ukusanyaji wa taka.

Amesema kuwa, licha ya changamoto nyingi zinazokabili sekta hiyo bado halmashauri inathamini kazi ya huduma zinazotolewa na Wazabuni hao, kwa wananchi na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia kanuni, sharia na taratibu na kujikita zaidi kwenye makubaliano yaliyomo kwenye mikataba ya zabuni zao.

Aidha Mkurugenzi huyo amewataka wananchi wote wanaopata huduma ya uzoaji taka katika maeneo yao, kulipia huduma hiyo kulingana na bei elekezi zilizotolewa na kufafanuliwa katika sheria ndogo za kuimarisha Afya na Usafi wa mazingira za Halmashauri hiyo.

“Huduma ya uzoaji taka katika mitaa, inalipiwa si huduma ya bure, niwatake wananchi kutoa ushirikiano kwa Wazabuni wa uzoaji taka pamoja na kutunza taka hizo mpaka pale gari litakapokuja kuzibeba” amesema Mkurugenzi huyo.

Hata hivyo wazabuni hao walizitaja changamoto zinazowakabili katika kazi ya ukusanyaji taka ikiwa ni pamoja na mazingira magumu ya kazi kutokana na changamoto ya ufinyu wa barabara na njia za kungia kwenye baadhi ya mitaa, gharama kubwa za uendeshaji na kutokulipwa kwa wakati na kuthibitisha kuwa, endapo changamoto hizo zitafanyiwa kazi na kulipwa fedha zao kwa wakati itasaidia kutatua changamoto hizo, na kuwawezesha kuzoa taka kwa wakati katika maeneo husika.

Licha ya changamoto hizo za uendeshaji, wazabuni hao wamelalamikia,  baadhi ya wanasiasa wanaowashawishi wananchi kutolipa fedha kwa ajili ya huduma ya uzoaji taka, jambo linalosababisha migogoro baina ya wananchi na wazabuni na  kukwamisha jithada hizo za kazi zao.

Hata hivyo mkurugenzi Mahera ameahidi kuwa ofisi yake kupitia Idara ya Usafishaji na Mazingira, kushirikiana na wazabuni hao kuweka mazingira bora kuanzia ngazi ya kijiji, kata na halmashauri kwa ujumla kuhakikisha zoezi hilo la uzoaji taka linafanyika kwa usahihi bila kuonea upende wowote kwa kusimamimia sheria ndogo za kuimarisha Afya na usafi wa Mazingira.

Aidha amewaonya wanasiasa wanaowarubuni wananchi na kuwashawishi kugoma kulipia huduma ya takataka na kusisitiza kuwa suala la uzoaji taka na usafi wa mazingira ni suala mtambuka lisilohitaji siasa.

" Wananchi mnapaswa kutambua uzoaji taka katika maeneo yenu ni kulinda afya zenu, athari za kinyume na hapo ni mlipuko wa magonjwa, ambao husababisha vifo, acheni kuwafuata wanasiasa wamaowarubuni, ulipiaji taka upo kisheria  hauhitaji siasa" amesisitiza Mkurugenzi Mahera

Awali, Sheria ndogo za usafi, kuimarisha Afya na usafi wa mazingira ya halmashauri ya Arusha ya mwaka 2010, kifungu nambari 29 kinaeleza wazi adhabu ya mtu yeyote atakaye kamatwa kwa kushindwa kulipa hela ya taka atatozwa faini ya shilling laki tatu 300,000 ua kufungwa miezi 12  au adhabu zote kwa pamoja.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.