• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI ACHENI UKATILI, CHANGIENI CHAKULA CHA WATOTO SHULENI

Posted on: September 19th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Wazazi wametakiwa kutimiza majukumu yao katika kulea watoto wao na kuacha kufanyia ukatili kwa mikono yao wenyewe, kwa kuacha kuwalipia watoto wao chakula cha mchana, wawapo shuleni, kwa dhana potofu ya kuwa, serikali inawahudumia watoto kwa kutoa elimu bure.

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Arusha, Dkt, Wilson Mahera, wakati akifungua warsha ya siku tatu ya Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto MTAKUWWA halmashauri ya Arusha, amesema kuwa, wazazi wamekuwa na tabia ya kuwafanyia ukatili watoto wao, kwa kuwanyima, chakuka cha mchana wawapo shuleni, kwa madai ya kuwa elimu ni bure, jambo ambalo ni kinyume na taratibu.

Ameongeza kuwa,serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali, wamekuwa mstari wa mbele kutetea haki za watoto na kupambana na ukatiti dhidi ya watoto lakini bado baadhi ya wazazi wamekuwa kikwazo kwenye harakati hizo, kwa kushindwa kwa makusudi kuwalipia chakula  cha mchana wawapo shuleni, kwa madai kuwa elimu ni bure, jambo ambalo linakwamisha juhudi za serikali pamoja na kudhorotesha kiwango cha ufaulu kwa watoto.

"Kwa tabia ya kutokumpa mtoto chakula cha mchana huo ni ukatili, haiwezekani mtoto kushinda na njaa, kuanzia asubuhi mpaka jioni akiwa shuleni, halafu useme unampenda mtoto wako, huo ni ukatili na unapaswa kuachwa mara moja" amesema mkurugenzi.

Aidha amewasihi wazazi kuwaonea huruma watoto wao,  na kutambua kuwa Sera ya elimu bila malipo, inaweka wazi majukumu ya serikali na majukumu ya mzazi kwa mtoto, ikiainisha jukumu la mzazi ni pamoja na kumpatia mtoto chakula cha mchana kwa shule za kutwa, kumpatia vifaa vya shule na mahitaji yake yote ya msingi.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Kijiji cha Watoto SOS, Grace Nkya, amesema kuwa shirika lake linajihusisha na kupambana na ukatili dhidi ya watoto kwa kuwalea na kuwahudumia, watoto wanaoshi kwenye mazingira hatarishi na kuwaundia familia ili aweze kuishi kama yuko nyumbani.

Nao wajumbe wa Kamati hiy ya MTAKUWA wamethibitisha kuwa moja ya changamoto inayowakabili wazazi ni kuweka viapumbele kwenye masuala yasiyo ya muhimu ambayo hugharimu pesa nyingi na kushindwa kukidhi mahitaji ya watoto.

Wamefafanua kuwa, wazazi wako radhi kuchangia fedha nyingi kwenye harusi na mbesii 'kumsalimia mtoto aliyezaliwa', na kushindwa kuchangi chakula cha mchana cha mtoto wake, jambo ambalo wamethibitisha ni ukatili unaofanywa wazi kabisa na wazazi.

"Ni rahisi kabisa, kutoa shilingi laki moja mpaka tano, kuchangia harusi au mbesii moja, na kutelekeza kulipia chakula cha mtoto cha shilingi laki moja kwa mwaka mzima" wamesema wajumbe hao.

Aidha wameitaka jamii sasa, kubadilika na kuanza kuwekeza fedha nyingi kwenye elimu na sio kwenye masuala ya kijamii, ambayo kimsingi ni ya muda mfupi na hayana tija kwa taifa letu la Tanzania.

Hata  hivyo, Afisa Ufisa Ustawi wa Jamii, mkoa wa Arusha, Denis Mgiye, amesema kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati ya MTAKUWWA wilaya, kupambana na ukatili dhidi ya watoto pamoja na kubadilishana changamoto zinazowakabili watoto.





Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.