• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI SHULE YA SEKONDARI MWANDET WAKABIDHI GARI KWA WALIMU WA SHULE HIYO 

Posted on: March 24th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Wazazi wenye watoto wanaosoma shule ya Sekondari Mwandet, halmashauri ya Arusha, wamekabidhi gari kwa shule hiyo, gari aina ya Coaster yenye namba za usajili T 169 DQX pamoja na kadi ya gari hilo, gari ambalo wamepanga litumiwe na walimu wa shule hiyo, kwenda na kurudi shuleni, makabidhiano yaliyofanyika shuleni hapo wakati wa mahafali ya 5 ya kidato cha sita 2022.

Wakizungumza wakati wa kukabidhi gari hilo, wazazi hao wamesema kuwa, wamesukumwa na changamoto kubwa ya usafiri, iliyokuwa inawakabili walimu wa shule hiyo ya namna ya kufika shuleni kila siku, na kuamua kichangishana fedha za kununua gari, litakalowawezesha walimu kufika shuleni kwa urahisi na kwa wakati.Mwenyekiti wa Kamati ya manunuzi ya gari hilo, Heveanlight Mushi, amesema kuwa, umoja wa wazazi wenye watoto wanaosoma shule ya sekondari Mwandet, wamewiwa kuchangishana fedha za kununua gari, kwa ajili ya walimu wanaowafundisha watoto wao, kutokana na kazi nzuri inayofanywa na walimu shuleni hapo, ya kuwafundisha wanafunzi huku wakiishi umbali mrefu kutoka shuleni hapo.

Mwenyekiti huyo, ameongeza kuwa, walimu wa shule ya sekondari Mwandet, wanajuhudi kubwa katika kuwafundisha watoto, na matokeo ya juhudi hizo yanaonekana wazi, jambo ambalo limetugusa wazazi wote, na kufanya maamuzi ya kuwanunulia gari, ili kuwarahisishia usafiri wa kufika na kuondoka shuleni kwa wakati.

"Shule ya Mwandeti ni kubwa, ina walimu wengi, haina nyumba za kutosha kuishi walimu wote hapo shuleni, lakini pia eneo hili halina nyumba za kupangisha, hivyo asilimia kubwa ya walimu hulazimika kuishi Ngaramtoni, huku kukiwa hakuna usafiri wa kuaminika kufika shuleni, walimu wanateseka sana, wazazi tumeamua kuwaondolea adha hiyo wakati wakiwahudumia watoto wetu" amesisitiza Mwenyekiti huyo.

Aidha amefafanua kuwa ununuzi wa gari hilo, umegharimu kiasi cha shilingi milioni 48, fedha zilizopatikana kwa kila wazazi kuchanga kiasi cha shilingi elfu thelathini, jambo ambalo limefanyika kwa muda wa miezi miwili, mara baada ya makubaliano ya wazazi wote.

Akizungumza wakati wa kupokea gari hilo mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kuwashukuru wazazi hao kwa, kuwanunulia walimu gari, amewapongeza wazazi hao, kwa moyo wa imani walionao wa kuthamini kazi kubwa inayofanywa na walimu kwa watoto wao, jambo ambalo wazazi wengi hawatambui wala kuthamini kazi hiyo kubwa inayofanywa na walimu.

Mkurugenzi Msumi, amefafanua kuwa, kutokana na Jiografia ya halmashauri ya Arusha, walimu wa shule nyingi za pembezoni wanakabiliwa na changamoto ya nyumba za kuishi pamoja na usafiri wa kufika shuleni, licha ya kuwa walimu hao, hujitoa kwa hali na mali, kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kufundisha wanafunzi kwa kuweka uzalendo mbele, hivyo wa wazazi hao wamefanya jambo kubwa sana kwa maendelo ya shule ya Mwandet na halmashauri kwa ujumla.

Aidha amewataka, wazazi wengine kuigana mfano huo uliofanywa na wazazi wa Mwandet sambamba na kuwataka wadau wa elimu, kujitokeza kuisaidi serikali kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu, hususani katika ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na usafiri.

"Licha ya kuwa serikali imejikita katika kuboresha miundombinu ya shule pamoja na ujenzi wa nyumba za walimu lakini bado kuna changamoto kubwa ya upungufu wa nyumba za walimu, ukilinganisha na idadi kubwa ya walimu waliopo, hivyo niwakaribishe wadau kuchangia ujenzi wa" amesisitiza Mkurugenzi Msumi

Hata hivyo mkuu wa shule sekondari Mwandet, mwalimu John Masawe, amewasukuru wazazi kwa kutambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na wallimu wa shule hiyo kwa kuwanunulia gari, litakalo rahisisha ussafiri kwa walimu na kuahidi kuendelea kusimamia walimu hao, kuchapa kazi na kupataa matokeo maazuri kwa wanafunzi ili waweze kutimiza ndoto zao.

Shule ya sekondari Mwandet ni miongoni mwa shule za kata, inayoendelea kukua kwa kasi, na kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa, huku ikiwa ni miongozi wa shule 10 bora kitaifa kwa miaka mitatu mfululizo kwa matokeo ya kidato cha sita.










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.