• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZEE WAMETAKIWA KUZIKUBALI CHANGAMOTO ZA UZEE NA KUKABILIANA NAZO....

Posted on: October 6th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Wazee halmashauri ya Arusha wametakiwa kuamini kuwa uzee ni baraka kutoka kwa Mungu hivyo kuwa tayari kuzikubali changamoto za utu uzima kwa kujiweka imara katika kukabiliana nazo kwa kuwa ni sehemu ya maisha ya uzee.


Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Dkt. Ojung'u Salekwa, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani 2023, yaliyofanyika kijiji cha Nduruma kata ya Nduruma ambapo zaidi ya wazee 400 walikusanyika kuadhimisha siku hiyo muhimu kwao.


Amesema kuwa umri unaposogea mwili unaanza kudhoofu na kusababisha kukubiliwa na changamoto nyingi za kijamii na kiuchumi jambo ambalo linasababisha uzee kuonekana kama ni tatizo na kuwasihi wazee kuzikubali na kutambua kuwa changamoto hizo ni sehemu ya maisha ya utu uzima, zisiwakatishe tamaa na kuona kuwa uzee ni tatizo, bali kujiweka imara kukabiliana nazo.


"Niwatie moyo wazee wangu, licha ya changamoto zinazowakabili, tambueni kuwa serikali ya awamu ya sita inatambua na kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na wazee katika kulijenga Taifa la Tanzania, kwa kuweka mazingira ya kuwahudumia wazee katika sekta mbalimbali pamoja na kuunda mabaraza ya wazee yanayotoa fursa ya kuwakutanisha na kubadilishana uzoefu kuanzia ngazi ya kata, wilaya, mkoa na mpaka Taifa". Amesema Mwenyekiti Ojung'u


Hata hivyo wazee hao licha ya kuishukuru serikali kwa jitihada za kuwajali na kuwahudumia, wamebainisha kuwa bado kuna changamoto za  upatikanaji wa Bima za afya, upatikanaji wa vitambulisho vya wazee, vitambulisho vya taifa (NIDA) pamoja na baadhi ya wazee kushindwa kujihudumia kutokana na hali duni za kiuchumi huku wakiiomba serikali kuwaingiza kwenye mpango wa TASAF.


Akisoma risala ya Baraza la  wazee, Katibu wa Baraza la Wazee halmashauri ya Arusha, Mzee Julias Marasi amesema kuwa bado idadi kubwa ya  wazee hawana vitambulisho muhimu ikiwemo vya Taifa na vya wazee hali inayowasababishia usumbufu mkubwa pindi wanapohitaji baadhi ya huduma kwenye ofisi za umaa na zile za binafsi na kuiomba serikali kushugulikia changamoto hizo ili wazee waendele kunufaika na matunda ya nchi hii.


Ameongeza kuwa wapo wazee ambao bado wana ngunvu hivyo ni vyema serikali ikaandaa mpango wa kuwawezesha kiuchumi kwa kuwapa mikopo isiyokuwa na riba kama yalivyo makundi mengine maalumu ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Awali Maadhimisho ya Siku ya Wazee yana lenga kuhamasisha jamii kuongeza uelewa wa juu ya masuala yanayohusu uzee na kuzeeka ikiwemo haki zao na upatikanaji wa huduma muhimu kwa wakati.


Kauli mbiu:"Udhibiti wa Wazee kwenye Dunia yenye mabadiliko"


ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.