• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI JENISTA: TUMIENI RASILIMALI WATU  ZILIZOPO  KWENYE HALMASHAURI ZENU BADALA YA KUSUBIRI SERIKALI KUAJIRI .

Posted on: October 13th, 2022

Na Elinipa Lupembe 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama, amewataka wakurugenzi kutumia rasilimali watu walizonazo katika halmashauri badala ya kusubiri serikali kuajiri watumishi.

Waziri Jenista ameyasema hayo, wakati wa kikao kazi cha siku moja kilichowakutanisha watumishi wa wailaya ya Arumeru yenye halmashauri mbili za Arusha na Meru, kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Meru.

Waziri ametoa rai hiyo mara baada ya wakurugenzi wa halmashauri hizo, kuwasilisha taarifa ya hali ya watumishi katika halmashauri hizo ikionyesha kuna upungufu wa watumishi katika kada za afya, walimu, manunuzi na wakaguzi wa Ndani kutokana na sababu mbalimbali.

Hata hivyo Waziri Jenista amewaagiza wakurugenzi, kutumia watumishi ambao tayari wako kwenye ajira kwa kuwaendeleza kitaaluma kulingana na uhitaji na baadaye kuwabadilishia kada ili kukidhi upungufu uliopo badala ya kusubiri serikali kuu kuajiri.

"Tengenezeni uwiano wa watumishi wetu, kuna kada ambazo kuna zidio la watumishi, watumieni hao kwa makubaliano ya kimaandishi, wekeni bajeti ya kuwaendeleza kitaaluma, halafu wabadilishieni kada, kwa kufanya hivyo tutapunguza hili tatizo lakini zaidi tutaipunguzia serikali mzigo wa kuwa na watumishi wanaolipwa kwa kufanya kazi kidogo" Amesisitiza Waziri Jenista.

Hata hivyo Waziri Jenista amewataka Maafisa Rasilimali watu, kusimamia haki za watumishi bila upendeleo, kwa kuhakikisha kila mtumishi anapata haki yake sawa na mwingine, huku akisisitiza kila mtumishi kutimiza  wajibu wake katika kutekeleza majukumu aliyopangiwa na mwajiri.

"Serikali imewaamini na kuwapa jukumu la kuwasimamia watumishi, wapatieni haki zao, ili tufikie lengo la serikali la kuwahudumia wananchi, mtumishi asipopata haki yake hata utendaji wake wa kazi unakuwa wa kulegalega, tunahitaji watumishi wenye kufanyakazi kwa weledi wakiwa na imani na serikali yao iliyowaajiri" Amesisitiza Mheshimiwa Waziri

Aidha Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango licha ya kumshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa ujio wake na somo alilolitoa kwa watumishi, ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo, maoni na ushauri kwa kuhakikisha halmashauri za wilaya ya Arumeru zinawahudumia watumishi kwa haki na usawa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

"Mheshimiwa Waziri leo tumeongeza maarifa  na uelewa mkubwa katika kutimiza wajibu na kutekeleza majuku ya kiutumishi, kwa maendeleo ya Taifa letu, umetukumbusha watumishi tuna deni kubwa kuwahudumia wananchi, tukuahidi hatutakuangusha wewe na mheshimiwa Rais, nikuahidi tutaendelea kushirikiana na Maafisa Utumishi, kuhakikisha tuna wasimamia watumishi kutekeleza majukumu yao na kufikia lengo la serikali la kuwahudumia wananchi" Amesisitiza Mkuu wa wilaya.

Naye Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu na Utawala, Halmashauri ya Arusha, Elizabeth Ngobei, amekiri kupokea maelekezo na kwenda kuyafanyia kazi kwa kuhakikisha watumishi wanatimiza wajibu wao na kuoata haki zao ili kuongeza tija na ufanisi katika kazi.

Awali Mheshimiwa Waziri, amefanya ziara ya siku moja katika wilaya ya Arumeru na kufanya kikao na Wakuu wa Ifara na Vitengo wa halmashauri za  Arusha na Meru pamoja na watumishi wa halamshauri ya Meru.



ARUSHA DC 

KaziInaendelea



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.