• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA, JAMII INAENDELEA KUELIMIKA KATIKA KUTOA TAARIFA YA MATUKIO YA UKATILI DHIDI YA WATOTO

Posted on: June 14th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2023,  kuna mafanikio ya uelewa wa jamii katika suala zima la Ulinzi na Usalama wa mtoto ambao unaongezeka siku hadi siku.

Akizungumza ofisini kwake na mwandishi wetu, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, halmashauri hiyo, Stedvant Kileo, amesema kwamba, licha ya changamoto za matukio ya ukatili dhidi ya watoto nchini, amefafanua kuwa, halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali imefanikiwa kuanzisha Kamati za Ulinzi na Usalama wa mtoto ngazi ya kata na Wilaya (MTAKUWWA), kamati zinazofanya kazi ya kuelimsha na kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa Ulinzi na Usalama wa mtoto kwa kuzingatia haki za mtoto zilizoanishwa na Umoja wa Mataifa na Mataifa ya Afika.

Aidha halmashauri imeweza kuanzisha klabu za kupinga ukatili kwa watoto shule za msingi na sekondari, klabu ambazo zinawapa fursa watoto wenyewe kujitambua, kutambua haki zao, kuyafahamu matukio ya ukatili pamoja na kujilinda dhidi ya ukatili sambamba na kutoa taarifa ya matukio ya kikatili dhidi yao.

"Tuna klabu 100 kwa shule za msingi na klabu 35 kwa shule za sekondari  pamoja na madawati ya kijinsia kwa shule zote, kwa pamoja zikiongozwa na walimu wa malezi wanaojengewa uwezo wa ulinzi na usalama wa mtoto mara kwa mara". Amefafanua Kileo.

Aidha halmashauri inashirikiana na taasisi za serikali ambazo ni wajumbe wa MTAKUWWA ngazi za kata na wilaya wakiwemo Jeshi la Polisi, Polisi kata, Dawati la kijinsia la Polisi, Maafisa Magereza, Maafisa Uhamiaji, wazee wa mila, viongozi wa dini pamoja na Mahakimu na weaendesha mashitaka wanaoushughulikia kesi za watoto kwa ufasaha na haraka.

Kupitia majukwaa hayo, jamii imeanza kuelimika na kuripoti matukio ya ukatili wanayofanyiwa watoto ndani ya jamii ikiwemo, ubakaji, ulawiti, ndoa za utotoni pamoja na watoto kutumikishwa jambo ambalo limewezesha watuhumiwa kukamwatwa na baadhi kutiwa hatiani na kuhukumiwa vifungo jela.

Hata hivyo amewataka wazazi na walezi wanaowapa watoto wao simu, kufuatilia maudhui wanayoyaangalia na kupakua kupitia simu hizo, kwa kuwa kupitia simu hizo, watoto wanajifunza maadili mabaya ambayo ni kinyume na mila na desturi za kitanzania.

 "Kufuatia Kauli Mbiu ya mwaka huu inamtaka mzazi na mlezi kuzingatia usalama wa mtoto katika ulimwengu wa Kidigitali, hivyo ni jukumu la wazazi na walezi kuwasimamia watoto juu ya matumizi ya simu janja na mitandao ya kijamii, kompyuta pamoja na  televisheni" Ameongeza Mkuu huyo wa Idara.

Kwa upande wake muendesha mashitaka Koplo Jane Mandu, kituo cha Polisi Ngaramtoni amesema kuwa kuanzia mwezi Januari mpaka Juni jumla ya matukio 23 yaliripotiwa huku kesi 8 zikitolewa hukumu, kesi  6 watuhumiwa wakihukumiwa kifungo cha maisha na kesi 2 wakihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.

Koplo Jane amesema kuwa licha ya jamii kuanza kuripoti matukio ya ukatili dhidi ya watoto, bado kuna changamoto ya wanajamii kushindwa kujitokeza kutoa ushahidi mahakamani kwa kuhofia kuharibu mahusiano yao na watuhumwa, kwa kuwa matukio mengi ya ukatili yanatokea nyumbani yakihusiha ndugu, jamaa na marafiki.

"Jeshi la polisi kwa kushirikiana na raia wema, wanajitahidi kufuatilia watuhumiwa wa matukio ya ukatili dhidi ya watoto lakini bado kuna baadhi ya mashahidi kutoka ndani ya jamii, kushindwa kutoa ushahidi jambo ambalo linasababisha baadhi ya watoto kukosa haki zao, pindi kesi zinapowasilishwa kwenye vyombo vya sheria". Amefafanua Koplo Jane.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.