• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WIZARA YA KILIMO KUPITIA MAMLAKA YA UDHIBITI WA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO (COPRA) YAZINDUA RASMI MSIMU WA UNUNUZI WA ZAO LA PARACHICHI KWA MWAKA 2025/2026

Posted on: September 27th, 2025

Wizara ya Kilimo kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imezindua rasmi msimu wa ununuzi wa zao la Parachichi kwa mwaka 2025/2026 huku ikisisitiza udhibiti wa ubora na uongezaji thamani ili kuongeza mchango wa zao hilo katika pato la Taifa na kuinua kipato cha wananchi.

Uzinduzi huo umefanyika tarehe 25 Septemba 2025, mkoani Njombe, ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka ambaye amesisitiza umuhimu wa wakulima kuuza zao la Parachichi kwa wakati ili kuepuka hatari ya mazao kuharibika na kupoteza ubora. Aidha, amebainisha kuwa hatua hiyo itawasaidia wakulima kupata bei nzuri na yenye tija, sambamba na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika masoko ya Kimataifa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Dkt. Stephen J. Nindi amesema Serikali imejipanga kuimarisha mnyororo wa thamani wa Parachichi, kuendeleza masoko ya Kimataifa na kukuza kilimo cha biashara chenye tija kwa wakulima.

Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa za uhifadhi, uongezaji thamani na utafiti, ili kuhakikisha Parachichi linalozalishwa Tanzania linaendelea kukidhi viwango vya Kimataifa. Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza ajira kwa vijana, kukuza ushindani wa bidhaa kwenye soko la Dunia na kuinua kipato cha wakulima mmoja mmoja.

Washiriki ambao ni pamoja na wakulima, wanunuzi, wasindikaji na wasafirishaji wa zao la Parachichi walipata fursa za kujadiliana namna bora ya kuendeleza Tasnia ya Parachichi, hususan katika kuongeza thamani, kuboresha ubora na kufungua fursa za masoko ya ndani na nje ya nchi.

Washiriki wengine walioshiriki ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), Bi Irene Mlolwa; Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uendelezaji wa Mazao ya Mbogamboga na Matunda (TAHA), Dkt. Jacqueline Mkindi; Wakuu wa Wilaya; na Wakurugenzi wa Halmashauri mbalimbali kutoka maeneo tofauti yanayolima zao la Parachichi nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA August 14, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA BW. SELEMAN MSUMI AWASHONEA SARE MADEREVA WA HALMASHAURI HIYO

    October 02, 2025
  • WIZARA YA KILIMO KUPITIA MAMLAKA YA UDHIBITI WA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO (COPRA) YAZINDUA RASMI MSIMU WA UNUNUZI WA ZAO LA PARACHICHI KWA MWAKA 2025/2026

    September 27, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ARUMERU MWINYI AHMED MWINYI AHITIMISHA MAFUNZO YA JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT)

    September 21, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA AWAASA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA USAFI

    September 21, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.