Na Elinipa Lupembe
Halmashauri ya Arusha, imeanza mkakati wa kutekeleza mpango jumuishi wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, kwa watoto wenye umri wa kuanzia miaka 5 mpaka 14, walioandikishwa shule na wasio kwenye mfumo wa shule.
Akizungumza wakati wa kikao kazi hicho, Katibu Tawala wilaya ya Arumeru, Mwl. James Mchembe, ameitaka timu ya watalamu iliyoteuliwa kuhakikisha wanafanya kazi hiyo kwa bidii na kwa kushirikiana ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
"Huu ni mpango wa kitaifa, tunatakiwa kuhakikisha tunatekeleza shughuli hii kila mmoja kwa nafasi yake, ili kufikia malengo ya serikali ya kuwakinga watoto ambao wako kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa ya minyoo tumbo ili kuwaandaa watoto kuwa na Taifa lenye watu wenye afya bora hapo baadaye". Amesisitiza Katibu Tawala huyo.
Aidha Katibu Tawala huyo, amewataka watalamu licha ya kutoa dawa kinga hizo, ni vema kujikita pia kutoa elimu ya usafi kwa jamii, ili kujikinga na minyoo kwa kuwa na vyoo bora pamoja na kuwa na tabia chanya za afya za kunawa mikono kwa maji safi na sabuni kabla ya kula, kabla ya kunyonyesha mtoto, wakati wa kumtawaza mtoto na mara baada ya kutoka chooni pamoja na watoto kuvalishwa viatu.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha, mhe. Ojung'u Salekwa, ameishukuru serikali kwa mpango huo mpango ambao una manufaa makubwa kwa watoto, wananchi na jamii kwa ujumla wake.
"Ninaipongeza serikali, ninamshukuru mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa na mpango wa kuandaa watoto wenye afya bora, watoto ambao ni wajenzi wa Taifa la kesho, mtoto asiyeshambuliwa na magonjwa afya yake ya akili inayomuwezesha mtoto kulitumikia taifa lake akiwa na afya bora" Amesisitiza Mwenyekiti Ojung'u
Mganga mkuu halmashauri ya Arusha, Dkt. Peter Mboya, ameweka wazi kuwa, halmashauri inategemea kutoa kinga tiba ya minyoo tumbo kwa watoto 80,000 wa kuanzia miaka 5 mpaka 14, walio kwenye mfumo wa shuleni na wasio kwenye mfumo wa shule.
Amefafanua kuwa makusudi ya mpango ni kuendeleza mpango jumuishi wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ukiwa na dira ya kuwa na jamii yenye afya bora na ustawi na usiyodhoofisha na madhara ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.
Mratibu wa magonjwa yasiyo ya kuambukizwa halmashauri ya Arusha, Ramadhani Kulewa, amesema kuwa halmashauri inategemea kutoa kinga tiba ya ugonjwa wa minyoo tumbo kupitia vituo 211, vituo vya afya 56 na kwenye shule za msingi 155 huku wahudumu 433 wakiwemi walimu 310 na wahudumu wa afya 112.
Kulewa aethibitisha kuwa ili kufikia lengo, licha ya kuwa na vituo hivyo maalum halmashauri pia itatumia mfumo wa ugawaji dawa katika jamii kwa kupita nyumba kwa nyumba, ugawaji wa dawa kwa makundi maalum, pamoja na kwenye mikusanyiko ya watu kama nyumba za ibada, sokoni, vituo vya mabasi na meeneo yote ya biashara.
Awali halmashauri ya Arusha inategemea kuwapatia kinga tiba ya minyoo kwa watoto 80,000, watoto 76,000 kati yao ni wale waliosajiliwa shuleni na watoto 4,000 ni ambao hawajasajiliwa kwenye mfumo rasmi wa elimu.
ARUSHA DC
KaziInaendelea
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.