• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Arusha DC yajipanga kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto

Posted on: March 14th, 2018

Halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru, imejipanga kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto unaotokana na mila na desturi potofu zinazoendelezwa ndani ya jamii.

Mikakati hiyo imeanza kwa kuunda kamati ya ulinzi na usalama wa wanawake na mtoto ngazi ya halmashauri, kufuatia mwongozo wa serikali wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati hiyo, kaimu mkurugenzi halmashauri ya Arusha, ndugu Paulus Kessy, amesema kuwa halmashauri imeunda kamati hii kwa lengo la kuhakikisha ulinzi na usalama wa wanawake na watoto kwa kutokomeza mila na desturi zinazowakandamiza.

Ameongeza kuwa suala la mila na destruri lina changamoto nyingi, hivyo kamati hii ina kazi kubwa ya kuelemisha jamii juu ya athari ya mila hizo kandamizi kwa kufuata kanuni, taratibu na sheria za serikali.

"Kamati inatakiwa kuwa na uhusiano chanya kati ya wazazi, walezi, watoto na jamii nzima, uhusiano wenye lengo la kuelimishana na kukemea mila potofu, uhusiano utakaowezesha halmashauri kufikia lengo la mwanamke na mtoto kupata haki " amesema Kaimu mkurugenzi

Aidha kaimu mkurugenzi Kessy ameweka wazi mikakati itakayotekelezwa na halmashauri hiyo ni pamoja na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa asilimia 50% ifikapo mwaka 2025 kwa jamii kujengewa uwezo wa kusimamia haki za wanawake na watoto.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii mkoa wa Arusha Theresia Costantine, ameainisha majukumu ya kamati hiyo ni pamoja na kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kushiriki katika utoaji huduma kwa makundi yaliyo katika mazingira hatarishi.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto utatekelezeka, endapo kamati itafanyakazi kwa ushirikiano kwa kumuweke na mtoto kwanza.

Hata hivyo Sumaiya Abdul (12) , mwenyekiti wa Baraza la watoto halmashauri ya Arusha ameonyesha kufurahishwa na uundaji wa baraza hilo kuongeza kuwa anaamini kupitia kamati hii watoto watapata haki zao za msingi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.