Na Elinipa Lupembe
Halmashauri ya Arusha imeendelea kung'ara katika mashindano ya michezo shule za sekondari UMISETA ngazi ya mkoa, kwa kuchukua jumla ya makombe manne, medali 6 za dhahabu, 3 za shaba na 1 ya fedha, huku wachezaji 20, wakichaguliwa kuwakilisha mkoa ngazi ya Taifa, mashindano yanayotegemea kufanyika mkoani Tabora.
Wakizungumza wakati wa kukabidhi makombe hayo kwa mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, kwenye ofisi za makao makuu ya halmashauri hiyo, wachezaji hao wamesema siri kubwa ya ushindi ni nidhamu na kufuata maelekezo ya makocha katika michezo.
Damian Christian mmoja wa wanariadha aliyeshinda medali ya dhahabu, amekiri siri kubwa ya mafanikio katika timu zao, ni kuwa na malengo, juhudi binafsi, nidhamu, ushirikiano pamoja na kufuata maelekezo ya walimu wao wakati wote wa michezo wakiwa kambini.
"Sisi kama wachezaji, tuliingia kwenye mashindano tukiwa na malengo ya ushindi, tukaweka juhudi na nidhamu, kwa pamoja zikatuwezesha kufikia lengo la ushindi na kupata makombe na medali hizi" Amesisitiza mwanariadha Damian.
Hata hivyo Mkurungenzi Msumi, licha ya kuwapongeza kwa ushindi huo mnene, ameonyesha kufurahishwa na uwakilishi mzuri wa wachezi hao kwa kuiwakilisha vema halmasahuri yao na kurudi na makombe na medali.
Aidha amewapongeza wachezaji 20 waliochaguliwa kuwakilisha mkoa ngazi ya Taifa, na kuwataka kuongeza bidii na nidhamu zaidi pamoja na kufuatilia maelekezo na mbinu za wanaozofundishwa na walimu, na kuwasisitiza kurudi na ushindi kama ilivyokuwa katika ngazi ya mkoa.
"Nidhamu ndio kila kitu, hivyo ninawaamini vijana wangu nendeni mkapambane kwa manufaa ya halmashauri yetu, mkoa wa Arusha pamoja na Taifa kwa ujumla, mnafahamu michezo ni ajira, hivyo jitahidini ili vipaji mlivyonavyo viweze kuwafikisha mbali zaidi katika kulitumika Taifa la Tanzania". Amesisitiza Mkurugenzi Msumi.
Naye Afisa Elimu Sekondari halmashauri ya Arusha, Mwl. Menard Lupenza amefafanua kuwa katika mashindano ya UMISETA ngazi ya mkoa, halmashauri ya Arusha ilipata ushindi wa kwanza kwenye michezo mitatu ya soka la wasichana, mpira wa Pete na wasanii wa kizazi kipya, ushindi wa pili kwenye Mpira wa wavu kwa wavulana na riadha wavulana, ushindi wa tatu Fani za ndani ngoma na kwaya, mpira wa kikapu wavulana na wasichana na mpira wa mikono kwa wavulana.
Ameongeza kuwa kwa matokeo ya jumla halmashauri imeshika nafasi ya nne na kufanikiwa kupata jumla ya makombe 4, medali 6 za dhahabu, 3 za shaba na 1 moja ya fedha, huku jumla ya wanamichezo 20 wakichaguliwa kuwakilisha mkoa kwenye mashindano ya UMISETA ngazi ya Taifa yenye Kauli mbiu ya "TAKWIMU SAHIHI NI MSINGI WA MIPANGO BORA YA TAIFA" SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI KWA MAENDELEO YETU" .
SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022
JIANDAE KUHESABIWA ✍✍
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, seleman Msumi, akiwa ameshikilia makombe na medali za ushindi wa UMISETA ngazi ya mkoa, mara baada ya kukabidhiwa na wachezaji 20 waliochaguliwa kujiunga na timu ya mkoa wa Arusha kushiriki UMISETA ngazi ya Taifa.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.