Na. Elinipa Lupembe.
Halmashauri ya Arusha, imeshika nafasi ya kwanza na kuzibwaga halmashauri sita, tasisi za umma na binafsi, mashirika ya Umma na binafsi, kwenye maadhimisho ya sikuu ya Wafanyakazi Duniani mkoa wa Arusha, yaliyofanyika katika viwanja vya General Tyre.
Akiwaongoza wafanyakazi wa halmashauri ya Arusha, mkurugenzi Mtendaji, Seleman Msumi, kupokea Kombe la ushindi wa kwanza, mbele ya mgeni rasmi, mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongela, amewashukuru na kuwapongeza watumishi wa halmashauri hiyo, kwa kujitoa kufanyakazi kwa bidii na kwa ushirikiano.
Mkurugenzi Msumi, amewahakikishia watumishi, utumishi uliotukuka kutoka kwake na kufungua milango ya majadiliano na mashauri mbalimbali yanayoweza kukwamisha ufanisi wa kazi katika eneo la kazi."Ninathamini na kutambua mchango mkunwa unaotokana na utumishi wa kila mmoja katika eneo lake la kazi, maendeleo yote yanayoonekana katika halmashauri yanatokana na uwajibikaji wa watumishi wa halmashauri ya Arusha" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.
Aidha amethibitisha kuyafanyia kazi maelekezo na maagizo yaliyotolewa na mkuu wa mkoa, wakati wa hotuba yake ya maadhimisho ya Sikukuu ya wafanyakazi mkoa wa Arusha.Wafanyakazi wa mkoa wa Arusha wameungana na wafanayakazi wote Duniani, kuadhimisha Sikukuu hii muhimu inayowakutaniasha wafanyakazi wote kwa pamoja, kuwasilisha changamoto na ufanisi wa majukumu yao sehemu za kazi kwa waajiri wao.
Kauli Mbiu ya MEI MOSI 2022 "Mishahara na Maslahi Bora kwa Wafanyakazi Ndiyo Kilio Chetu", Kazi iendee, ikionesha namna wafanyakazi wana ari ya kufanya kazi inayokwenda sambamba na mishahara na maslahi bora kwa wafanyakazi wa sekta zote.
ARUSHA DC
#KaziInaendelea✍✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.