Na Elinipa Lupembe
Halmashauri ya Arusha imeshika nafasi ya pili kwa kuwa halmashauri bora kwenye maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi Mei Mosi 2023 na kukabidhiwa kombe la ushindi huo.
Ushindi huo umetangazwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John Mongela, wakati wa sherehe za Mei Mosi 2023 mkoa wa Arusha, zilizofanyika kwenye viwanja vya Shekh Amri Abeid Jijini Arusha.
Akizungumza mara baada ya kupoke Kikombe hicho, Mkrugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kushukuru kwa kupata tuzo hiyo, amebainisha kuwa, ushindi huo ni alama ya uwajibikaji wa watumishi wa halmashauri yake, na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingati Kanuni,Sheria na Taratibu za Utumishi wa Umma.
"Tunao wajibu mkubwa wa kuwahudumia wananchi, kupitia zawadi hii, mimi na watumishi wenzangu tunakwenda kufanya maradufu, jukumu letu kubwa ni kuwatumikia wananchi wa halmashauri ya Arusha, kupitia zawadi hii, tumejipanga kwa upya" .Amesema Mkurugenzi Msumi
Wafanyakazi wa halmashauri ya Arusha licha ya kufurahia kupata zawadi hiyo, wamesema kuwa, imewaongezea ari ya kufanyakazi kwa juhudi na maarifa zaidi, huku wakiahidi kuweka mbele maslahi ya wananchi wa halmashauri hiyo.
"Zawadi hii ina thamani kubwa sana kwetu, ni chachu katika kuchapa kazi, imetupa ari ya kwenda kuchapa kazi ya kuwahudumia wananchi ili kufikia malengo ya Serikali kwa maendeleo ya Taifa letu, tupo tayari na tumejipanga" Wamebainisha Watumishi wa halmashauri hiyo.
Sherehe za Mei Mosi 2023, zimefanyika nchi nzima huku Kitaifa zikifanyika mkoani Morogoro, mgeni rasmi akiwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kauli mbiu 2023: "Nidhamu na bidii ya kazi ndio msingi wa mafanikio kazini"
ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.