• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ARV KUENDELEA KUPATIKANA BURE, KICHEKO KWA WATUMIAJI

Posted on: February 21st, 2025

ARV KUENDELEA KUPATIKANA BURE, KICHEKO KWA WATUMIAJI



Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, amesema kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha huduma za dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI (ARV) zinapatikana bure kwa WAVIU wote.


Dkt. Mollel ametoa kauli hiyo Februari 20, 2025, wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya Mradi wa Timiza Malengo mkoani Lindi, uliozinduliwa na Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Ummy Deriananga, kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.


Mhe. Dkt. Mollel amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kiasi kikubwa, ikiwa ni pamoja na uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya afya pamoja na upatikanaji wa dawa zikiwemo dawa za kufubaza virusi vya UKIWMI (ARV)

"Serikali imetumia zaidi ya Shilingi Bilioni 48 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya, ikiwa ni pamoja na hospitali, vituo vya afya na zahanati katika mkoa wa Lindi na maeneo mengine nchini," amesema Dkt Mollel


Aidha, Dkt. Mollel amesisitiza kwamba Serikali itaendelea kufanya kila juhudi kuhakikisha kwamba huduma za afya zinawafikia Watanzania wote bila ubaguzi, huku akiwahimiza wananchi kuwa na utamaduni wa kupima afya zao ili kuepuka magonjwa yanayoweza kuzuilika.


Pia, Dkt. Mollel amesema kwa sasa huduma za kibingwa, ikiwemo matibabu ya uvimbe wa ubongo bila kupasua kichwa na matibabu ya kansa ya ubongo kwa kutumia sauti maalum, zinapatikana nchini Tanzania ambapo upatikanaji wa huduma hizo za kibingwa hapo awali zilikuwa zikipatikana kwa shida au kutoonekana kabisa.


Mradi wa Timiza Malengo awamu ya tatu unalenga kuboresha sekta ya afya na unasimamiwa katika halmashauri 36 za mikoa 10 ya Tanzania Bara, ambapo mikoa ya Dodoma, Geita, Lindi, Mara, Morogoro, Njombe, Ruvuma, Singida, Tabora, na Tanga inahusika.


Mradi huu unalenga kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya na kuboresha mazingira ya huduma za afya kwa wananchi wote, huku Serikali ikijitahidi kutekeleza malengo ya kuleta maendeleo kwa wananchi, hasa wale walioko maeneo ya vijijini.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.