• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ASAS YA AAIDRO YAZINDUA MRADI WA MILIONI 230 KUWAINUA WANANCHI WA HALI YA CHINI KIUCHUMI

Posted on: November 29th, 2022


Na Elinipa Lupembe.

ASAS ya Kiraia ya AAIDRO ya kanisa Katoliki Jimbo Kuu Arusha chini ya Idara ya Jinsia na Wanawake imezindua mradi wa kuwainua wananchi wenye hali ya chini kiuchumu katika kata za Nduruma na Bwawani Halmashauri ya Arusha.

Akizungumza wakati wa kuutambulisha mradi huo, kwenye ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, kwa niaba ya Kanisa Katoliki Padri  Faustine Moshi, amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha mwaka mmoja na utahusisha makundi rika tofauti kwa lengo la kuwawezesha wananchi kijiinua kiuchumi na kijamii.

Aidha Padri Mosha amesema kuwa Kanisa limeona ni vema kushirikiana na Serikali kuwahudumia wananchi katika sekta nyingine zaidi ya ile ya kiroho, na kuongeza kuwa wanatarajia kupata ushirikiano mkubwa kutoka kwa watalamu wa halmashauri ili kufikia lengo la kanisa na malengo ya serikali ya kuwahudumia wananchi.

“Utekelezaji wa mradi huu utagharimu takribani shilingi milioni 230 na kuwajengea uwezo watu 200 kupitia vikundi, hivyo ni matumaini yetu, kazi hii itafanywa na kanisa na watalamu kutoka serikalini kupiti halmashauri, kwa pamoja tutafikia lengo”.Amesisitiza Padri Mosha.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amelishukuru Kanisa kupitia ASAS ya AAIDRO kwa kuona umuhimu wa kuunga mkono juhudi za serikali za kuwajengea uwezo wananchi kujikwamua kiuchumi, kazi ambayo ingefanywa na serikali.

“Kama Hamashauri tuko tayari kushirikiana na kanisa kwa kuzingatia jukumu la serikali ni kuweka mazingira rafiki kwa mashirika yanayofanya kazi za kuhudumia jamii kulingana na mpango mkakati wa serikali, tunao watalamu wa kutosha katika idara zote, hivyo watashirikiana nanyi katika hatua zote za utekelezaji wa mradi huu”. Amesbainisha Mkurugenzi Msumi.

Aidha amelitaka shirika hilo Kwenda kutekeleza mradi huo kulinga na andiko la mradi na si vinginevyo, sambamba na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kila robo ya mwaka kwenye vikao vya kisheria vya mashirika yasiyo ya kiserikali.

Naye mratibu wa mradi huo, Irene Moshi, amefananua kuwa mradi huo utajikita katika kuwapa mafunzo wakulima na kufanya kilimo cha kisasa, kilimo biashara kulingana na Ajenda 10/30, kuwajengea uwezo wajasiriamali pamoja na masuala mtambuka ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanaume, wanawake na watoto ikiwemo ukeketaji na ndoa za utotoni.

“Kupitia mradi huu tunategemea kuwaiwezesha jamii kuwa na uwezo wa kujikomboa kifkra, uwezo wa kujitegemea kiuchumi katika kujipatia pato la familia, pamoja na kuwa na jamii huru isiyokuwa na ukatili wa aina yoyote katika masuala ya kijinsia”. Amesistiza Irene

Awali kwa sasa mradi huo uko katika hatua za awali, utatekelezwa kwa muda wa mwaka mmoja na unategemea kukamilika ifikapo Juni 2023.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.