• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BALOZI KOMBO ASHIRIKI KIKAO CHA 46 CHA BARAZA LA MAWAZIRI AU

Posted on: February 13th, 2025

BALOZI KOMBO ASHIRIKI KIKAO CHA 46 CHA BARAZA LA MAWAZIRI AU


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amewasili jijini Addis Ababa, Ethiopia ambapo anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Kikao cha 46 cha Baraza la Mawaziri la Umoja wa Afrika (AU) kinachofanyika tarehe 12 na 13 Februari, 2025.

Kikao cha Baraza la Mawaziri kilitanguliwa na Kikao cha 49 cha Kamati ya Mabalozi/Wawakilishi wa Kudumu kwenye Umoja wa Afrika kilichofanyika kuanzia tarehe 14 Januari hadi 10 Februari, 2025 ambapo vikao hivyo ni maandalizi ya awali ya Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika utakaofanyika Addis Ababa, Ethiopia tarehe 15 na 16 Februari, 2025.


Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika na ataambatana na Mawaziri na Viongozi wengine Waandamizi kutoka katika Wizara, Idara na taasisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Pamoja na masuala mengine Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika utachagua na kuidhinisha Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika pamoja na Makamishna sita (6) wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika baada ya viongozi waliopo sasa kumaliza muda wao wa miaka 4 (2021-2025) wa kuhudumu katika Kamisheni hiyo; kuchagua na kuidhinisha wajumbe watano (5) wa Baraza la Amani na usalama la Umoja wa Afrika; Kuchagua mjumbe mmoja (1) wa Taasisi ya Anga ya Afrika; na kuchagua na kuidhinisha nafasi ya Makamu wa Rais wa Baraza la Chuo Kikuu cha Pan-African.


Uchaguzi mwingine ni wa wajumbe watano (5) wa Bodi ya Ushauri Dhidi ya Masuala ya Rushwa ya Umoja wa Afrika, Uchaguzi wa mjumbe mmoja (1) wa Kamati ya Wataalamu Afrika inayoshughulikia Haki na Ustawi wa Mtoto na uchaguzi na uteuzi wa wajumbe sita (6) wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika katika Sheria ya Kimataifa.


Vilevile, Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali utapitia na kujadili ripoti za masuala ya kimkakati ikiwemo: Ripoti ya Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika; Ripoti kuhusu

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.