• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CCM ARUMERU WAUTAKA UONGOZI ARUSHA DC KUANDAA SITE PLAN KATIKA MAENEO YOTE YA UMMA

Posted on: July 7th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Uongozi wa halmashauri ya Arusha, umetakiwa kuanza kuandaa mpango wa matumizi ya maeneo yote ya umma 'site plan' ili kuwa na mpango bora wa matumizi bora ya maeneo hayo kwa sasa na miaka ijayo.

Rai hiyo imetolewa na Wajumbe wa kamati ya Siasa wilaya ya Arumeru, wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya siku mbili ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri ya Arusha, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mwenyekiti wa halmashauri hiyo. 

Wajumbe hao waketoa agizo hiloo baada ya kujionea ongezekomlamlasi la ujenzi wa majengo yanayojengwa katika maeneo ya shule za msingi na sekondari, majengo ambayo yanadhihirisha wazi kuwa kukosekana kwa mpango wa matumizi, kutasababisha kuwa na majengo yasiyo n mopangilio katika maeneo hayo ya Umma.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, mheshimwa Simon Ole Saning'o amesema kuwa ni vyema halmashauri ikaanza utaratibu wa kuandaa mpango wa matumizi ya maeneo 'site plan', katika maeneo yote ya umma ikiwemo shule, hospitali, vituo vya afya na zahaanati, lengo likiwa ni kuwa na majengo ambayo yamepangwa katika eneo husika.

"Serikali inatoa pesa za kujenga miundombinu katika ssekta za elimu na afya, kutokana na kasi ujenzi wa majengo, anzeni kuwa na 'site plan' za maeneo hayo ili kuondoa hali ya majengo holelaa yasio na mpangilo, kkama ni eneo la shule kuwe na plan inayoonyesha eneo la madarasa, vyoo, nyumba za walimu, viwanja na sio kuwa na majengo holela'amesisitiza Mwenyekiti huyo wa CCM Arumeru.

Hata hivyo Maenyeki huyo amesema kuwa uwepo wa mpago wa matumizi ya maeneo ya umma uende sambamba na ujenzi wa majengo ya magorofa, ujenzi ambao utazingatia ufinyu wa ardhi katika halamshauri yaArusha, na kuongeza kuwa, uwepo wa majengo yaliyo kwenye mpangilio mzuri katika maeneo ya Umma, licha ya kuwa na muonekano mzuri lakini pia utachangia matumizi bora ya arddhi.

Aidha mheshimwa Saning'o, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutoa pesa kwa ajili ya kuteleleza miradi mbalimbali kisekta, miradi ambayo inadhihirisha utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapiinduzi  iliyonadiwa wakati wa uchaguzi  mkuu wa mwaka 2020.Aidha amewataka wananchi wa Arumeru, kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mheshimiwa mama Samia Suluhu Hassan kwa kuifanya kazi kwa bidii huku waakilinda amani iliyopi kwa maendeleo ya taifa la Tanzania.

Hata hivyo Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa licha ya kuishukuru Kamati ya Siasa kutembelea na kukagua shughuli za utekelezaji wa miradi ya maendeleo inahotekelezwa katika halamshauri hiyo, amesema kuwa halamshauri imepokea maelekezo hayo na kuanza kuyafanyia kazi kwa haraka  na kuongeza kuwa tayari halamshauri imeanza kuandaa mipango ya matumiza ya maeneo ya umma 'site plan'  na wanaendelea kukamilisha maeneo ambayo bado.

Awali Kamati ya  siasa wilaya ya Arumeru, imefanya ziara ya kukagua jumla ya miradi 12 yenye thamaniya shilingi milioni 637, fedha zilizotolewa na serikali kuu, ziara yenye lengo  la kufuatailia utkelezaji wa Ilaani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 -2025.


ARUSHA DC 

KAZI IENDELEE✍

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Aruemeru Mhe. Simon Ole Saning'o akizungumza kwenye kikao cha majuisho, baada ya ziara ya Kamati ya Siasa wilaya ya Arumeru kukagua miradi ya maenedleo halmashauri ya Arusha, kwenye ukumbi wa mikutano wa Mwenyekiti wa halamshauri hiyo.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.