• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA CWCD LAZINDUA PROGRAMU YA KUWATETEA WATOTO WA KIUME

Posted on: September 26th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Shirika lisilo la kiserikali la Center for Women and Children Develepment (CWCD) limezindua mradi wa kuwatetea watoto wa kiume, kwa kuanzisha klabu za wavulana kwenye shule za msingi 6, unaojulikana kwa jina la Maabara ya watoto wa kiume shuleni 'BOY'S VAC LAB'.

Akiwasilisha taarifa ya mradi huo, mkurugenzi wa shirika la CWCD, Hindu Mwego, amesema kuwa, shirika limekuja na mradi wa kuwawezesha watoto wa kiume kujitambua na kutambua haki zao kama ilivyo kwa watoto wa kike,, kutokana na ukweli kwamba, watoto wa kike wamekuwa wakitetewa na kuwaacha nyuma watoto wa kiume ambapo madhara yake yameanza kujitokeza sasa kwenye jamii.

Ameongeza kuwa, Takwimu za Jeshi la Polisi za mwaka 2021, zinaonyesha kati ya matukio ya ukatili 391 yaliyoripotiwa, matukio 312 ni matukio ya ulawiti kwa watoto wa kiume, huku takwimu zikishuka kwa watoto wa kike hali iliyolisukuma shirika kuanza programu ya kuwahudumia watoto wa kiume.

"Kwa takwimu hizi, ni dhahiri kuwa jamii imejikita kuwatetea watoto wa kike huku watoto wa kiume wakiachwa nyuma, jambo ambalo linasababisha watoto wa kiume kufanyiwa vitendo vya ukatili huku jamii ikiona kuwa watoto hao wana uwezo wa kujitegemea, jambo ambalo sio sawa, watoto wa kiume nao wanapaswa uangalizi na kutetewa kama ilivyo kwa watoto wa kike". Amesisitiza mama Hindu

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi licha ya kulishukuru shirika hilo, amethibitisha uwepo wa ongezeko la matukio ya ulawiti kwa watoto wa kiume, huku jamii ikijikita zaidi kumlinda mtoto wa kike.

Ameongeza kuwa, kwa sasa jamii inalazimika kuanza mkakati wa kuwatetea watoto wote, kwa kuwa hata watoto wa kiume wana haki ya kulindwa kama ilivyo kwa watoto wa kike.

"Tumeanza kuona matokea ya kuwatetea na kuwalinda  watoto wa kike peke yake, na kuwaacha watoto wa kiume wakijitegemea kimakuzi, na matokeo yake yameanza kujitokeza, kwa sasa tunashuhudia makundi ya vijana wadogo wakijiingiza kwenye vitendo vya uhalifu, kama ilivyo kwa vijana wanaojiita panya road  ambapo hivi karibuni wamekuwa wakijeruhi watu, kupora Mali zao na hata kuua watu wasio na hatia". Amefafanua Msumi

Hata hivyo watoto walioshiriki mafunzo hayo, wamefurahishwa na mradi huo, kwa kuweka wazi kuwa ni kweli watoto wa kiume wamekuwa wakiachwa nyuma, hivyo kuanza mkakati wa kuwalinda na kuwatetea wavulana utaleta matunda mema kwa jamii.

Simplisit Siprian, mwanafunzi wa darasa la (5) shule ya msingi Ngaramtoni, amesema kuwa kuna umuhimu wa kuwatunza na kuwatetea watoto wa kiume, kwa kuwa nao wanahitaji kulindwa kama ilivyokuwa watoto wa kike.

"Watoto wa kiume wasiachwe nyuma, wapewe haki sawa na watoto wa kike, kushindwa kufanya hili kunasababisha wavulana kujiingiza kwenye makundi ya kiuhalifu kwenye jamii, vijana wavulana ndio wanapora na kuiba mali za watu pamoja na kuua watu mitaani". Amefafanua mwanafunzi Simplisiti.

Naye Mratibu wa Dawati la Jinsia na mpelelezi wa kesi za ukatili, kituo cha Polisi Ngaramtoni, Koplo Jane Kitundumandi, amethibitisha uwepo wa matukio ya ukatili kwa watoto na ulawiti kwa watoto wa kiume katika jamii yetu, na kuitaka jamii kutoa ushirikiano wa kuwa wakweli na wawazi katika kutoa ushahidi ili kuwatetea watoto na kuhakikisha wanapata haki zao dhidi ya ukatili wanaofanyiwa.

"Changamoto kubwa inayokwamisha kesi za ukatili dhidi ya watoto ni mila na desturi za kimaasai, kwa kufanya vikao vya usuluhishi kwenye familia zao nyumbani, usuluhishi unaokwamisha ushahidi na watoto wengi kupoteza haki zao, lakini kwa sasa tutatumia nguvu hata kwa mashahidi ili kufanikisha kesi hizo". Amefafanua Koplo Jane

Shirika la CWCD, linafanya kazi za kijamii ndani ya halmashauri ya Arusha kwa kutoa huduma za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwenye kata 19 za halmashauri hiyo huku mradi wa 'Boy's Vac Lab' ukitekelewa kwenye shule 6 za msingi za Moivo, Naurei, Olturoto, Ilboru, Kiranyi na Ngaramtoni. kwa ufadhili wa shirika la Foundation For Civil Society.


ARAUHA DC

KaziIendelee✍✍









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.