• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DANIDA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WATOTO ARUSHA DC.

Posted on: November 8th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Shirika la Maendeleo ya Kimàtaifa la nchini Denimaki (DANIDA) limeridhishwa na kupongeza utekelezaji wa mradi wa kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto, unaotekelezwa katika halmashauri ya wilaya ya Arusha, mradi unaofadhiliwa na mfuko huo, kupitia ASAS ya Foundation For Civil Society na kutekelezwa na ASAS ya Center for Women and Children Development (CWCD) ya Arusha.

Wadau hao wa maendeleo, wameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo, mara baada ya kutembelea baadhi ya klabu za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto, katika shule ya msingi Ilboru  kitengo cha elimu maalum na klabu ya wasichana shule ya sekondari Ilkiding'a na kujionea namna watoto walivyojengewa uwezo wa kujitambua, kutambua haki na wajibu wao, kujithamini, kutambua aina za ukalitili, kupinga ukatili pamoja na kutoa taarifa pindi wapofanyiwa ukatili.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya shirika la Foundatio for Civil Society, Sosthenance Sambua, amethibitisha kuridhishwa na utekelzaji wa shughuli zinazofanywa na halmashauri kupitia miradi inayofadhiliwa na DANIDA kupitia FCS na kusistiza kuwa, kujionea namna watoto wa kike wanavyojiamini na uwezo wa kujitegemea kupitia mafunzo ya ujasiriamali, hali inaonyesha namna gani kazi nzuri inafanyika.

"Ujuzi mlioputa, tumieni kwa kuwaelimisha wasichana wengine shule na hata nyumbani kwenye jamii zenu, lakini nikuombe mkurugenzi kupitia Baraza la Madiwani, kuanza kuwa mipango mikakati ya kupata rasilimali za kuendeleza uwepo wa klabu za watoto shuleni, hata pale ambapo miradi ya wafadhili itafikia ukomo" amesistiza Sambua 

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mheshimiwa Ojungu Salekwa, amekiri kuwa jamii anayotokea yeye ni  waathirika wakubwa wa ukatili wa wanawake na watoto unaotokana na mila na desturi za kabila lao la kimasaai, ila wao kama viongozi wa jamii, wako mstari wa mbele kupambana na ukatili huo kwa kuelimisha jamii yao, kuachana na mila hizo potofu, zinazoathiri kwa kiasi kikubwa maendeleo ya wanawake na familia kwa ujumla.

Mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kuwashukuru wadau hao wa maendeleo, ameahidi kuendelea kusimamia vema utekelezaji wa miradi hiyo ili iwe endelevu kwa faida ya sasa na vizazi vijavyo na kuongeza kuwa serikali inaweka mazingira rafiki kwa wadau, kwa kuwa inathamini  michango ya wadau, michango ambayo kimsingi inatekeleza malengo na mikakati ya serikali kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

"Serikali inaweka mazingira rafiki kwa wadau wa maendeleo wa ndani na nje yanchi, lengo likiwa kuwapa fursa kushirikiana na serikali kusukuma gurudumu la maendeleo, niwashukuru sana DANIDA kwa miradi ya kupinga ukatili wa kijinsia, mnayoifadhili katika halmashauri ya Arusha, miradi ambayo inaleta matoke chanya hasa kwa watoto wa kike, watoto ambao, walionekana ni wanyonge katika jamii" amesisitiza  mkurugenzi Msumi.

Klabu hizo za watoto shuleni, zimeonesha mafanikio makubwa sana kwa wanafunzi wasichana, kwa kuleta mapinduzi ya  kijamii na hata kitaaluma pia, wanafunzi wa kike wameweza kujifunza stadi mbalimbali za maisha, ikiwemo ujasiri wa kupinga ukatili, namna ya kukabiliana na changamoto za usichana, afya ya uzazi kwa vijana, ujasiriamali, stadi ambazo zimepunguza mimba shuleni, ndoa za utotoni, utoro shukeni na kupandisha kiwango cha taaluma kwa watoto wa kike.

Mwenyekiti wa klabu ya wasichana, shule ya sekondari ya  Ilkiding'a Maurine Philip kidato cha (IV), ameweka wazi kuwa, klabu ya wasichana shuleni, imewajengea wasichana uwezo wa kuwa wajasiri katika maamuzi, katika masomo yao na kuthibitisha kuwa wasichana wengi kwa sasa wameamua kupambana kujikita kwenye masomo ya Sayansi na wa wanafanya vizuri jambo ambalo hapo awali wasichana waliogopa kusoma masoma ya Sayansi.

"Tukiwa kwenye klabu, tunafundishwa masuala ya kijamii pamoja na ujasiliamali unaotuwezesha kutengeneza taulo za kike, kwa ajili yetu na wasichana wengine wasio na uwezo, lakini pia klabu imewezesha wasichana hata wasio kwenye kalabu kuwa active katika masomo, wasichana wengi wanafanya vizuri kwenye amsomo na hata katika masomo ya Sayansi, masomo ambayo zamani wasichana wengi tulikuwa tunayaogopa sana" amesistiza mwanafunzi Maurine.

Hata hivyo, ziara hiyo ilivuta hisia kali pale walipokutana na klabu ya watoto wenye ulemavu wa kusikia kitengo maalum, shule ya msingi Ilboru, waliojengewa uwezo wa kujiamini wakifanya igizo la ukatili kwa walemavu pamoja  na mabango yaliyokuwa na jumbe mbalimbali zikielezea kujiamini kwao, na jamii iwaamini kwamba wao wanafundishishika na wanauwezo wa kufanya kazi kama watu wengine.

Arusha DC KaziInaendelea✍✍









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.