• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU :

Posted on: May 23rd, 2023


Na Elinipa Lupembe

Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO's)  halmashauri ya Arusha yametakiwa kufanya kazi kwa kufuata taratibu na kuzingatia vigezo na vipaumbele vya maendeleo ya Taifa, kushindwa kufanya hivyo mashirika hayo yatachukuliwa hatufa za kisheria ikiwemo kungiwa kutoa huduma katika wilaya hiyo.

Hayo yamewekwa wazi na mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, wakati akifungua mkutano wa  mwaka wa mashirika (NGO's), uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya  Arusha, na kuwasisitiza kufanya kazi kwa kufuata taratibu.

Mkuu huyo wa wilaya ameyasisitiza mashirika hayo kuibua miradi kwa kuzingatia changamoto za jamii na kuitekeleza miradi hiyo kama iliyoanishwa kwenye maandiko ya mradi na si vinginevyo huku akiwata kutekeleza miradi yenye tija kwa jamii.

Amesema kuwa sheria ziko wazi kila shirika linatakiwa kuishirikisha serikali shughuli zote zinazofanyika  kuanzia ngazi ya wilaya halmashauri, kata, vijiji na vitongoji na kuwasilisha taarifa hizo kila robo ya mwaka kwa mkurugenzi kupitia msajili wa mashirika wilaya.

"Nisisitize mashirika yote yanayofanyakazi kwenye wilaya yetu, kuhakikisha mnafanyakazi kwa kushirikisha serikali kwa ngazi zote, ni utekelezaji wa majukumu yenu kufanya miradi yenye tija kwa kuzingatia vipaumbele vya Taifa, hatutasita kusitisha kazi za NGO ambayo inayotekeleza miradi isiyo na tija kwa jamii yetu" Amesisitiza mkuu huyo wa wilaya.

Hata hivyo Mkuu huyo wa wilaya ameyapongeza mashirika hayo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kushirikiana na serikali kuhudumia jamii ambayo inakabiliwa na changamoto nyingi kiseka.

" Kazi yenu ni bora sana, serikali inatambua na kuthamini sana kazi za mashirika, jambo la msingi ni kufuata sheria na taratibu bila kuathiri maadili ya watanzania na Taifa kwa ujumla, fanyeni miradi yenye tija kwa nchi yetu na si vinginevyo" Amesema Mhe. Emmanuela.

Naye Msajili Msaidizi wa NGO's halmashauri ya Arusha, Ahadi Mlai amesema sheria na taratibu za kuendesha mashirika ziko wazi, licha ya kushirikisha serikali kwa ngazi zote, ila shirika linatakiwa kufanya kazi kwa uwazi  kwa kuhakikisha jamii yote inafahamu mradi unaotekelezwa na manufaa yake katika maeneo wanayotekeleza mradi.

"Kabla ya kutekeleza mradi lazima waombe kibali kwa serikali, kwa kuonyesha gharama za mradi, muda wa utekelezaji, eneo la utekelezaji na umuhimu wa mradi huo kwa jamii, kutangaza mradi kwa jamii husika ili kila mwanajamii afahamu kinachoendelea katika eneo lao" Amefafanua Mratibu huyo.

Zaidi ya NGO's 40 zimesajiliwa kufanya kazi katika Halmashauri ya Arusha, yakiwa yamejikita katika kuhudumia jamii kwenye sekta za afya, kilimo na mifugo, ujasiriamali, Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii.

Awali mashirika yasiyoya kiserikali yamekutana na kufanya mkutano wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli zao kwa kipindi cha mwaka uliyopita wa 2022, mkutano ambao unafanyika kwa mujibu wa sheria, zinazoyasimamia mashirika hayo nchini.

ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.