Na Elinipa Lupembe.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, amefungua mkutano wa ITU SG 20, unakutanisha Wataalamu wa Kimataifa Kujadili Maendeleo ya Teknolojia duniani.
Mkutano huo wa siku 10, umeanza rasmi leo tarehe 13 Septemba, 2023, unafanyika kwenye Hoteli ya Grand Melia Jjiji la Arusha, umewakutanisha pamoja watalamu wa Teknolojia na Mawasiliano kutoka zaidi ya nchi 200 duniani kwa lengo la kujadili maendeleo na changamoto zinazohusiana na teknolojia za mawasiliano na habari katika ngazi ya kimataifa na kimataifa.
Akifungua mkutano huo kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. Emmanuela licha ya kuwakaribisha watalamu wa nchi wanachama duniani, amesema kuwa , mkutano huo ni fursa kwa nchi ya Tanzania kwa kuwapa nafasi watalamu kujifunza na kubadilishana uzoefu kutoka kwa nchi nyingine na kushirikiana ujuzi katika uga wa IoT.
"Kupitia mkutnao huu tunategemea wataalamu na wabunifu kutoka Tanzania wanapata nafasi ya kujadiliana na watalamu wenzao kutoka nch8 nyingi duniani, jambo ambalo litasaidia kuchangia kwa haraka maendeleo ya teknolojia nchini kwa kuinganisha Tanzania na nchi nyingine duniani". Ameweka wazi Mkuu huyo wa wilaya.
Awali Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Kundo Mathew, ameweka wazi umuhimu wa IoT na miji smart katika kuongeza ufanisi wa huduma za jamii na kiuchumi unaenda sambamba na ubora wa maisha ya wananchi wa Tanzania na dunia kwa ujumla wake.
Amesema kuwa nchi ya Tanzania imeonyesha dhamira ya kushirikiana na nchi nyingine katika kubadilishana ujuzi na maarifa na kusambaza uzoefu katika mawanda ya kiteknolojia duniani.
"Pamoja na majadiliano ya IoT na miji smart, mkutano huu unajumuisha masuala mengine muhimu ikiwa ni pamoja na usalama wa mifumo ya IoT na faragha, ulinganifu wa teknolojia , na faida za kiuchumi zinazotokana na maendeleo ya kijamii "
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari, amesema mkutano unaonesha dira ya kuchangia katika kuimarisha uchumi wa Tanzania.
#KaziInaendelea✍✍✍
PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.