• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AWAAGIZA WATAALAMU WA AFYA KUJIANDAA KUKABILIANA NA UGONJWA WA EBOLA.

Posted on: October 23rd, 2022

Na Elinipa Lupembe 

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango amewaagiza wataalamu wa afya wa halmashauri ya Arusha kufanya maandalizi mapema ili kuweza kukabiliana na ugonjwa wa Ebola ambao hivi karibuni mlipuko wake umetokea katika nchi jirani ya Uganda.

Mhandisi Ruyango ametoa maagizo hayo wakati wa kikao cha kamati ya afya ya msingi halmashauri ya Arusha kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo ambapo kimejumuisha viongozi wa dini na mila pamoja na wadau mbalimbali ili waweze kuwa mabalozi wa kutoa elimu hiyo waliyoipata katika maeneo wanapofanyia shughuli zao.

Aidha amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa changamoto kama vile upungufu wa rasilimali, dawa, vifaa tiba na kinga, ni muhimu kufanya maandalizi mapema na kuiandaa timu maalum ya ufuatiliaji pamoja kuelimisha Umma juu ya hatari ya ugonjwa huu na namna ya kujikinga.

.“Tukumbuke ugonjwa huu hauna tiba bali kinga na unaenea kwa haraka hivyo sisi kama Halmashauri ni vyema kuchukua tahadhari mapema ikiwemo kufanya ukaguzi wa afya kwa wageni wanaoingia nchini hasa katika mipaka isiyo rasmi na kuandaa vituo maalumu kwaajili ya kufanya vipimo vya ugonjwa huo”. Alisisitiza Mhandisi Ruyango.

Naye Mjumbe wa kamati ya Afya halmashauri ya Arusha Dkt. Japhet Champanda wakati akiwasilisha taarifa ya utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo amesema kuwa, Kila mwananchi anawajibika kuchukua tahadhari za kujikinga na kuwakinga wengine juu ya ugonjwa huu ikiwa ni pamoja na kuepuka kugusa wanyama kama vile popo, nyani, sokwe, tumbili na swala au mizoga ya Wanyama pamoja na kuzingatia usafi wa mazingira na usafi binafsi.

Hata hivyo wajumbe waliohudhuria kikao hicho wameipongeza halmashauri ya Arusha kwa niaba ya Serikali kwa hatua walizokwisha kuzichukua za kukabiliana na ugonjwa huo huku wakishauri elimu iendelee kutolewa katika mikusanyiko ya watu kama vile mikusanyiko ya kimila, makanisani, misikitini, mashuleni na minadani ili wananchi wapate elimu hiyo na wajue namna ya kujikinga.

"Ni vyema kila mtu kwa Imani yake amlilie Mungu ili aweze kutuepusha na janga hili huku elimu ikiendelea kutolewa bila kuleta taharuki kwa jamii ili kila mtu apate uelewa juu ya ugonjwa huu wa Ebola”. Alisistiza Mchungaji Pivs Edward Stevan, wa Kanisa la Naioth Gosple Assembly.

Mganga Mkuu Halmashauri ya Arusha Dkt. Petro Mboya ameweka wazi kuwa Halmashauri hiyo kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Arusha wametenga kituo cha afya Moshono kwa ajili ya kufanya matibabu ya wagonjwa waliogundulika na ugonjwa huo pamoja na eneo la TPRI kwaajili ya kuwatenga wahisiwa na waliokuwa karibu na wagonjwa wa Ebola.

Ifahamike kuwa ugonjwa wa Ebola unaosababishwa na Kirusi aina ya Ebola chenye anuwai sita uligundulika kwa mara ya kwanza mwaka 1976 katika nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Sudan na dalili za ugonjwa huo ni kama vile kupata homa kali ya ghafla, maumivu ya kichwa, Maumivu ya mwili, misuli na viungo, Kuharisha kunakoweza kuambatana na damu, Kutapika damu, Vipele mwilini, Kuvia damu chini ya ngozi au kutokwa na damu puani , mdomoni , machoni na masikioni.


JIKINGE NA  UGONJWA WA EBOLA, WAKINHE NA WENGINE

ARUSHA DC

KaziIendlee✍✍


















Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.